Pages


Home » » Mulugo amewajia juu wanaotaka yeye na Waziri wa Elimu Dk. Shukuru Kawambwa kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne.

Mulugo amewajia juu wanaotaka yeye na Waziri wa Elimu Dk. Shukuru Kawambwa kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne.

Kamanga na Matukio | 01:51 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga, Mbeya. NAIBU Waziri na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo amewajia juu wanaotaka yeye na Waziri wa Elimu Dk. Shukuru Kawambwa kujiuzulu nyadhifa zao kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne kwa kile alichodai wanaosema hivyo hawajui mfumo wa uongozi ulivyo.
 
Mulugo aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na Umoja wa Wamiliki, Mameneja na Wakuu wa Vyuo visivyokuwa vya Kiserikali ambapo alisema watu hao hawajui Nyadhifa za Waziri na Naibu Waziri kuhusu wajibu wao  pamoja na sekta zingine kama Tamisemi ambao na Wamiliki wa Vyuo.
 
Mulugo alisema Kazi ya Waziri na Naibu wake ni kusimamia Sera za Elimu na si vinginevyo na kuongeza kuwa jukumu la Walimu na wanafunzi na namna ya ufundishaji iko katika ngazi zingine ambayo ni Tamisemi na idara ya ukaguzi wa Shule.
 
Alisema Kazi yake yeye ni kuajiri Walimu na kuwakabidhi kwenye Halmashauri ambazo ziko chini ya Wizara ya Tamisemi hivyo suala la yeye kujiuzulu limeingizwa kisiasa kutokana na kulengwa watu wawili tu na kuziacha Sekta zingine.
 
Aliyataja baadhi ya mambo ambayo yamechangia kufeli kwa wanafunzi kwa kiasi kikubwa kumetokana na Wizara ya Elimu pamoja na baraza la Mitihani kuziba mianya na udanganyifu wa baadhi ya Walimu na Wamiliki wa Shule kununua Mitihani kabla haijafanyika.
 
Alisema baada ya kuziba mianya hiyo atakayebainika kufanya hivyo watafungiwa Shule zao ikiwa ni pamoja na kuchukuliwa Hatua za Kisheria kwa kupelekwa mahakamani na kufukuzwa kazi kwa wahusika.
 
Alitaja Sababu zingine kuwa ni Nidhamu kupungua kwa wanafunzi ambapo wanafunzi wanafika Shuleni kwa muda wanaoutaka ikiwa ni pamoja na kumiliki simu ambazo zinasababisha wanafunzi kujikita katika mitandao ya kijamii zaidi nakushindwa kuzingatia masomo.
 
Alisema ili nidhamu iweze kurudi na wanafunzi waweze kusoma kwa bidii ni kurudisha adhabu ya viboko au nyingine ambayo itasaidia wanafunzi kupenda Shule na kusoma kwa bidii na kuongeza kuwa Sera ya adhabu inabidi iangaliwe upya ili kurudisha Heshima ya Elimu kama ilivyokuwa awali.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger