Pages


Home » » Wakazi Chunya wasitisha uuzwaji wa kifusi cha mchanga kwa kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Mining Company Lt d

Wakazi Chunya wasitisha uuzwaji wa kifusi cha mchanga kwa kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta Mining Company Lt d

Kamanga na Matukio | 01:54 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Wakazi wa kijiji cha Saza wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wamesitisha uuzwaji wa kifusi cha mchanga kwa kampuni ya uchimbaji madini  ya Shanta Mining Company Ltd  kutokana na kutaka kuongezwa kwa  kiwango cha fedha kilichotolewa

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Saza wamesema kuwa kampuni hiyo imetoa dola za kimarekani laki mbili na hamsini elfu kununua kifusi hicho na kuahidi kulipa dola mbili kwa kila tani hali ambayo hawakukubaliana nayo

Wamesema kiwango cha dola mbili ni kidogo na kutaka kuongezwa dola nne kufikia sita hali ambayo mwekezaji alikataa na kuamua kukirudisha kifusi hicho kwa serikali ya kijiji

Akiongelea suala hilo mwanasheria wa serikali katika halmashauri ya wilaya ya Chunya Simanyani Twavusitile amesema wanaweza kuunda kamati ya mpito kwa ajili ya kukamilisha mchakato na tathimini ya kupata mteja mwingine kwa bei itakayokubalika.

Miongoni mwa Waliochaguliwa ni Tabia Andembwisye,Charles Andemwisye,Shadrack Machalawe,Atuganile Njala Robert Nselu, mtendaji wa kijiji John Ntakoma na mwenyekiti wa kijiji cha saza Philipo Mwakitalim.

Wakati huohuo Viongozi wa serikali ya  kijiji cha Saza wilaya ya Chunya mkoani Mbeya wanatuhumiwa kuuza eneo la kijiji kwa mwekezaji wa kampuni ya uchimbaji madini  ya shanta maining bila kuwashirikisha wakazi na halmashauri ya wilaya ya chunya

Wakizungumza na Chimbuko Letu baadhi ya wakazi wa kijiji hicho wamesema viongozi hao waliuza eneo hilo juni 17 mwaka 2009 kwa kiasi cha shilingi milioni mbili ambapo mwekezaji huyo amefanya eneo hilo kuwa makazi ya kudumu

Wamesema eneo lililouzwa lina ukubwa wa mita za mraba mia nne ambapo zimewekwa alama (BEACON)

Katika mkataba uliyosainiwa na viongozi hao na mwekezaji huyo unaonyesha kuwa haujapitishwa kwa mwanasheria ,mkurugenzi na raisi ambaye ndiye mwenye dhamana ya mwisho kwa uuzwaji au umiliki wa ardhi.

Viongozi wanaotuhumiwa kuuza eneo hilo ni pamoja na mwenyekiti wa kijiji Gasper Roki Msuwila, mtendaji wa kijiji Mariaam Mwanijembe, mjumbe wa kamati John Mpozayo  na mashahidi wawili ambao Meck Kitalawe na Christian Mambwe.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger