Pages


Home » » TAARIFA KUTOKA TFF: MPIRA KATI YA TAIFA STARS NA CAMEROON WAINGIZA MILIONI 148/-

TAARIFA KUTOKA TFF: MPIRA KATI YA TAIFA STARS NA CAMEROON WAINGIZA MILIONI 148/-

Kamanga na Matukio | 03:29 | 0 comments


Pambano la kirafiki la kimataifa kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Cameroon (Indomitable Lions) lililochezwa Februari 6 mwaka huu na wenyeji Stars kuibuka na ushindi wa bao 1-0 limeingiza sh. 148,144,000.  


Fedha hizo zimepatikana kutokana na watazamaji 23,092 waliokata tiketi kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 20,000 na sh. 30,000. 
 
 
Mgawanyo wa mapato hayo ulikuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 22,598,237.29, maandalizi ya mchezo sh. 58,000,000 wakati wa gharama za uchapaji tiketi ni sh. 7,340,900. 
 
 
Nyingine ni bonasi kwa wachezaji wa Taifa Stars sh. 18,831,864.41, asilimia 20 ya gharama za mchezo sh. 8,274,659.66, asilimia 15 ya uwanja sh. 6,205,994.75 na asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 2,068,664.92. 
 
 
Asilimia 60 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 24,823,978.98 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,241,199 ambayo ni asilimia 5 kutoka kwenye mgawo wa TFF.

Shirikisho la soka nchini TFF limetoa shukurani kwa wadau wote wa michezo waliotoa mchango uliopelekea uliopelekea ushindi wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars dhidi ya timu ya taifa ya Cameroon hapo 
Afisa habari wa TFF Boniface Wambura amesema hawana budi kutoa shukurani kwa wadau wa michezo nchini kutokana na ushindi uliopatikana wa bao moja kwa sifuri katika mchezo wa kimataifa wa kirafiiki ambao inaaminika itaisaidia Tanzania kupanda katika viwango vya ubora wa soka duniani.
Wakati TFF wakitoa shukurani hizo, uongozi wa klabu ya Simba nao umeipongeza timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars kwa kufanya vyema katika mchezo dhidi ya Cameroon.
Afisa habari wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga amesema bila kujali itikadi za ushabiki, uongozi wa klabu hiyo umeona ipo haja ya kuwapongeza wachezaji wote pamoja na viongozi wa benchi la Ufundi wa Taifa Stars kufuatia jitihada walizozionyesha na kupelekea furaha kwa watanzania.
Mchezo ulikua na lengo la kuiandaa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars ambayo inakabiliwa na mtihani wa kusaka nafasi ya kucheza fainali za kombe la dunia za mwaka 2014, ambapo mwezi ujao itacheza dhidi ya timu ya taifa ya Morocco ili hali timu ya taifa ya Cameroon itakabiliana na timu ya taifa ya Togo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger