Pages


Home » » Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari amesema hajaudhika sana na hatua hiyo ya kufungwa na Uingereza.

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari amesema hajaudhika sana na hatua hiyo ya kufungwa na Uingereza.

Kamanga na Matukio | 03:28 | 0 comments

Beki wa Timu ya taifa ya Uingereza Ashley Cole akipambana na mchezaji wa Timu ya Taifa ya Brazil Oscar. Uingereza waliibuka na usindi wa Goli 2 kwa goli moja

Habari Kamili. 
Baada ya kuanza vibaya akiwa na kikosi cha timu ya taifa ya Brazil ambacho kilishindwa kuunguruma katika uwanja wa Wimbely huko nchini Uingereza kufuatia kisago cha mabao mawili kwa moja kilichotolewa na wenyeji, kocha mkuu wa mabingwa mara tano duniani timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe Scolari amesema hajaudhika sana na hatua hiyo ya kufungwa. 


Luiz Felipe Scolari ambae alikiwezesha kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kutwaa ubingwa wa dunia mwaka 2002 huku akikiondoa kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza katika mchezo wa hatua ya robo fainali mwaka huo, amesema kwa sasa timu ya taifa ya Uingereza imebadilika na hana budi kukubaliana na suala hilo.


Amesema uzuri wa kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza umempa changamoto kubwa ya kukifanyia marekebisho kikosi chake, ambacho kitakua mwenyeji wa fainali zijazo za kombe la dunia kwa ajili ya kuhakikisha kinatoa upinzani kwa yoyote watakaekutana nae kwenye fainali hizo.


Wakati Luiz Felipe Scolari akikubalia matokeo ya kufungwa mabao mawili kwa moja kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uingereza Roy Hodgson amekipongeza kikosi chake kwa kusema kilicheza vizuri wakati wote huku kikifuata maelekezo yake.


Roy Hodgson ambae anajukumu zito la kubadili mwenendo wa timu ya taifa ya Uingereza, amesema walipambana na timu yenye vigezo vyote hivyo walichukua tahadhari mapema kwa kujiandaa kikamilifu na mwishowe walifanikisha azma waliyokua wameikusudia.



Wakati huo huo mshambuliaji wa klabu ay Man Utd Wayne Rooney amesema kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza kinastahili kujipongeza kwa ushirikiano mzuri ulioonekana kwa mashabiki wao na pia amesisitiza hali hiyo kuendelezwa kila wanapokutana na timu yoyote duniani.


Amesema hawana budi kufanya hivyo kutokana na soka kuwa katika mtazamo tofauti na ilivyokua siku za nyuma hivyo, ni jukumu lao kuhakikisha wanaendeleza mshikamano walionao kwa sasa.



Mabao ya timu ya taifa ya Uingereza katika mchezo huo wa kimataifa wa kirafiki yalipachikwa wavuni na Wayne Rooney pamoja na Frank Lampard katika dakika za 26 na 60 huku bao la kufutia machozi la timu ya taifa ya Brazil likifungwa na mshambulaiji wa klabu ya Fluminense Frederico Chaves Guedes.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger