Pages


Home » » Serikali wilayani Rungwe mkoani Mbeya imesema inatarajia kuanza kutoa vocha za Ruzuku kwa wakulima kupitia vikundi.

Serikali wilayani Rungwe mkoani Mbeya imesema inatarajia kuanza kutoa vocha za Ruzuku kwa wakulima kupitia vikundi.

Kamanga na Matukio | 02:45 | 0 comments


Mkuu wa wilaya ya Rungwe Crispin Meela
 Na Gabriel Mbwille, Mbeya.
 Serikali wilayani Rungwe mkoani Mbeya imesema inatarajia kuanza kutoa vocha za Ruzuku kwa wakulima kupitia vikundi ili kukabiliana na tatizo la wizi kutoka kwa mawakala na baadhi ya watendaji wa Serikali.



Akiongea na Mwandishi wetu Mkuu wa wilaya ya Rungwe Crispin Meela amesema mfumo wa awali ulikuwa ukitoa mwanya kwa mawakala kuwarubuni wakulima kwa kuwapa fedha badala ya pembejeo husika.



Kuhusu sababu ya Vocha kuchelewa kutolewa kwa wakati Meela amesema imetokana na mahitaji ya vocha hizo kuongezeka.



Wakati huohuo amesema Serikali imedhamiria kuwachukulia hatua za kisheria wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiwalaghai wakulima kwa kununua mazao yakiwa mashambani.



Aidha amesema ili kukabiliana na tatizo la wakulima kushawishika kuuza mazao yao yakiwa shambani Serikali imeanza kutoa mikopo yenye masharti nafuu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger