Pages


Home » » Kamati ya uchaguzi ya shirikisho al soka nchini TFF imeendelea kutupiwa lawama .

Kamati ya uchaguzi ya shirikisho al soka nchini TFF imeendelea kutupiwa lawama .

Kamanga na Matukio | 01:55 | 0 comments
Na Shaban Kondo,
Kamati ya uchaguzi ya shirikisho al soka nchini TFF imeendelea kutupiwa lawama baada ya kukamilisha zoezi ya kusikiliza mapingamizi yaliyowasilishwa na wadau wa michezo dhidi ya wagombea nafasi mbalimbali za uongozi wa shirikisho hilo.

Kamati hiyo baada ya kulaumiwa na Frank Mchaki aliekua amemuwekea pingamizi Hamad Yahya Juma anaewania nafasi ya mwenyekiti wa bodi ya ligi kuu pamoja na Saidi Mohamed anaewania nafasi ya makamu mwenyekiti wa bodi hiyo, imeendelea kulaumiwa na Paul Muhangwa Makoye aliekua amewawezkea pingamizi Mugosha galibona pamoja na Vedustas Lufano wanaowania nafasi ya ujumbe wa kamati ya utendaji ya TFF kupitia kanda ya pili (Mwanza na Mara).

Hata hivyo Paul Muhangwa Makoye ameweka wazi dhumuni la kusonga mbele katika kamati ya rufaa, kwa ajili ya kuisaka haki yake ambayo anaiona ni ya msingi kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa na kamati ya uchaguzi.

Wakati huo huo mwenyekiti wa klabu ya Azam FC Said Muhammed Abeid pamoja na Frank Mchaki wametangaza hatua ya kuendeleza uhusiano wao wa kuendeleza soka na kuyaacha masuala yote ya pingamizi baada ya kukutana kwenye kika cha kusikiliza pingamizi.

Said Mohamed ambae aliwekewa pingamizi na Frank Mchaki amesema suala hilo kwake limeshamalizika hivyo lililo mbele yake ni kuendeleza soka.
 
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger