Pages


Home » » Aliekua kocha mkuu wa klabu ya Simba Milovan Circovic, amesema asingependa kuifikisha klabu hiyo mbele ya FIFA, kwa kigezo cha kushindwa kumlipa malipo anayodai

Aliekua kocha mkuu wa klabu ya Simba Milovan Circovic, amesema asingependa kuifikisha klabu hiyo mbele ya FIFA, kwa kigezo cha kushindwa kumlipa malipo anayodai

Kamanga na Matukio | 02:43 | 0 comments
Aliekua kocha mkuu wa klabu ya Simba Milovan Circovic, amesema asingependa kuifikisha klabu hiyo mbele ya shirikisho la soka duniani FIFA, kwa kigezo cha kushindwa kumlipa malipo anayoudai uongozi wa klabu hiyo baada ya kusitishiwa mkataba wake mwishoni mwa mwaka 2012.


Milovan Circovic, ambae yupo nchini tangu juma lililopita kwa ajili ya kusaka haki yake ambayo aliahidiwa angelipwa mara baada ya fedha za usajili wa mshambuliaji kutoka nchini Uganda Emmanuel Okwi zitakapowasili kutoka nchini Tunisia, lakini amesema amekua akizunguushwa kila anapohitaji msaada wa kukutana na viongozi wa klabu hiyo kongwe hapa nchini.


Katika hatua nyingine kocha huyo kutoka nchini Serbia ameonyesha kusikitishwa na mwenendo wa kikosi cha simba tangu alipoondoka nchini kwa kusema, viongozi wa klabu hiyo wamefanya makosa makubwa kuharibu mipango aliyokua amejiwekea ndani ya timu hiyo, na matokeo yake hali imeendelea kuwa mbaya zaidi ya alivyoiacha.

 

Wakati Milovan Circovic, akidai kilicho halali kwake kutokana na kusitishiwa mkataba uongozi wa klabu ya simba umekiri ni kweli unadaiwa na kocha huyo aliewapa ubingwa msimu wa mwaka 2011-12, lakini wameukana ujio wake kwa kusema hawakumuarifu aje nchini kwa ajili ya kulipwa pesa zake kwa sasa.


Afisa habari wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga amesema suala la kocha huyo lipo wazi na kila siku amekua akielezwa kwamba pesa za usajili wa Emmanuel Okwi zitakapowasili kutoka nchini Tunisia atalipwa stahiki zake.

 Wakati huohuo Uongozi wa klabu ya Simba umekanusha taarifa za kuwa na mifarakano na baadhi ya wachezaji kama inavyoelezwa katika vyombo mbalimbali vya habari, hatua mbayo inachukuliwa kama chanzo cha kuendelea kufanya vibaya katika michezo ya ligi inayowakabili kwa sasa. 


Afisa habari wa klabu ya Simba Ezekiel Kamwaga amesema hakuna ukweli wa jambo hilo ambalo limechukua nafasi kubwa katia vyombo vya habari tangu mwishoni mwa juma lililopita na badala yake kikosi chao kipo katika hali nzuri baada ya kumaliza mchezo dhidi ya Oljoro JKT ulioshuhudia wakilazimishwa matokeo ya sare ya bao moja kwa moja.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger