Pages


Home » » Zaidi ya wanafunzi 70 wa Kidato cha Sita wamehitimu elimu ya juu ya Sekondari katika shule ya WENDA HIGH SCHOOL.

Zaidi ya wanafunzi 70 wa Kidato cha Sita wamehitimu elimu ya juu ya Sekondari katika shule ya WENDA HIGH SCHOOL.

Kamanga na Matukio | 18:53 | 0 comments
Picha na Habari na Yustina David, Mbeya..
Zaidi ya wanafunzi 70 wa Kidato cha Sita wamehitimu elimu ya juu  ya Sekondari katika shule ya WENDA HIGH SCHOOL ambapo katika mahafari hayo wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani yao wametunukiwa vyeti na zawadi mbalimbali.

Akiongea na wazazi pamoja na wahitimu mgeni rasmi wa mahafari hayo Padre Bazile Mzena amewahasa wanafunzi hao kumkumbuka Mungu katika masomo yao ili waweze kufikia malengo yao.

Sherehe za mahafali ya 4 ya Kidato cha sita shule ya Sekondari Wenda iliyopo Mbalizi zafana viongozi wa dini wahimiza wanafunzi kujituma katika masomo ya Sayansi.

Wanafunzi wa Wenda High School wakionesha umahili wao katika somo la Sayansi ambapo hapa wanaonesha namana walivyobobea katika uchanganyaji wa kemikamikali.

Mgeni Rasmi Padre Bazil Mzena ambaye ni mkuu wa Seminary ya Mafinga, akimsikiliza mwanafunzi wa Wenda High School aliyekuwa akimweleza umuhimu wa kujifunza masomo ya Sayansi na matarajio yake mara baada ya kuhitimu Kidato cha sita.


Hapa wanafunzi wakionesha mafanikio yaliyopatikana katika jaribio la kumpasua Panya.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger