Pages


Home » » Mtu mmoja auawa kwa wivu wa kimapenzi mkoani Mbeya.

Mtu mmoja auawa kwa wivu wa kimapenzi mkoani Mbeya.

Kamanga na Matukio | 18:52 | 0 comments
MWILI WA MAREHEMU DANIEL MWASALEMBA 30 UKIWA UMELALA KWENYE MAJANI BAADA YA KUCHOMWA KISU NA KUANGUKA MITA CHACHE KUTOKA NYUMBANI KWA ELIZABETH MICHAEL (18) KUTOKANA NA WIVU WA KIMAPENZI WA KUMGOMBANIA ELIZABETH MICHAEL.
ANAYEDHANIWA KUSABABISHA KIFO  CHA DANIEL  AMEJULIKANA KWA JINA MOJA TU PETER YEYE NI MWENYEJI WA SUMBAWANGA NA NA NIMWOSHA MAGARI YA KAMPUNI YA MABASI YA SUMRY JIJINI MBEYA AKIWA AMEPATA KIPIGO TOKA KWA WANANCHI WENYE HASIRA KALI
HAPA PETER AKIOKOLEWA NA WANAUSALAMA WALIOWAHI ENEO HILI LA TUKIO ASUBUHI HII
MWENYEKITI WA MTAA WA ITIJI EZEKIEL KING ALIYESIMAMA MLANGONI AKINESHA MICHILIZI YA DAMU KUTOKA KATIKA CHUMBA ALICHOMWA KISU MAREHEMU DANIEL KINACHOMILIKIWA NA ELIZABETH.
NDUGU WA MAREHEMU WAKIANGUA KILIO MARA BAADA YA KUONA MWILI WA NDUGU YAO DANIEL
HAKIKA ILIKUWA KAZI KUBWA SANA KWA POLISI KUMUOKOA PETER ANAEDHANIWA KUMUUA DANIEL KUMUOKOA KATIKA MIKONO YA WANANCHI WENYE HASIRA KALI
ANAEDHANIWA KUMUUA DANIEL AKIWA AMELALA CHINI BAADA YA KIPIGO KIKALI TOKA KWA WANANCHI WENYE HASIRA KALI

POLISI TAYARI WAMEUCHUKUA MWILI WA MAREHEMU DANIEL  HABARI KAMILI MBEYA YETU ITAZIDI KUKUJUZA KWANI BADO TUPO ENEO LA TUKIO 

HABARI NA PICHA NA EZEKIEL KAMANGA, MBEYA.
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Daniel Mwasalemba  mwenye umri wa miaka  30  mkazi wa Itiji  jijini Mbeya amefariki dunia baada kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa kimapenzi



Akizungumza na mtandao huu mwanamke aliyesababisha ugomvi huo Elizabeth Michael mwenye umri wa miaka 18  amesema marehemu alikuwa na ugomvi na mtu alifahamika kwa jina moja la Peter mkazi wa eneo hilo.



 Amesema ugomvi huo ulianzia katika kilabu cha pombe za kienyeji ambapo marehemu  alimsindikiza Elizabeth nyumbani kwake ndipo mtuhumiwa alipofuatilia na kumkuta nyumbani kwa Elizabeth na ugomvi kuanza saa nane usiku hali iliyopelekea mtuhumiwa kumchoma marehemu kisu na kumsababishia kifo chake



Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Balozi wa Mtaa huo Dotto Mwakasagule amesema baada ya kupata taarifa za marehemu kuuwawa kaika eneo lake alianza kufuatilia damu kutoka katika eneo la tukio hadi kwa Elizabeth na kumkamata Elizabeth wakati alipokuwa akipiga deki kuondoa damu.



  Hata hivyo mtuhumiwa alinusurika kuuwawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kukamatwa muda mfupi katika makaburi ya Nonde ambapo aliweza kuokolewa na jeshi la polisi baada ya kufyatua risasi hewani.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger