Pages


Home » » Tutaifunga Man U na kuiondosha katika 16 bora ya UEFA - Cristiano Ronaldo...

Tutaifunga Man U na kuiondosha katika 16 bora ya UEFA - Cristiano Ronaldo...

Kamanga na Matukio | 03:09 | 0 comments


Moto wa mchezo wa hatua ya 16 bora, unaosubiriwa kwa hamu kubwa na karibu mashabiki wote ulimwenguni kati ya Man Utd dhidi ya Real Madrid umeanza kuchakata kichwa ni aliekua mshambuliaji wa mashetani wekundu  Cristiano Ronaldo dos Santos Aveiro baada ya kuuzungumzia kwa hisia mpambano huo.



Cristiano Ronaldo ambae kwa sasa ni mshambuliaji wa kutumainiwa wa kikosi cha Real Madrid ameonyesha hali hiyo kutokana na mazungumzo yake alipohojiwa na vyombo vya habari nchini Ureno mara baada ya kuwasili kwa ajili ya kujiunga na timu ya taifa.



Ronaldo mwenye umri wa miaka 28 amesema ana kikosi cha The merengues kitafanikiwa kuwabwaga Man utd katika mchezo huo ambao utaanza kuunguruma Estadio Stantiago Bernabeu mnamo Februari 13 kabla ya kumaliziwa huko Old Trafford March 05.



Hata hivyo mshambuliaji huyo ambae alisajiliwa kwa ada ya uhamisho wa paundi million 80 iliyoweka rekodi mpaka sasa ameendelea kusisitiza kwa kusema anatambua Man Utd kwa sasa ndio vinara wa ligi kuu ya nchini Uingereza na wana timu nzuri, lakini suala hilo haliwatishi zaidi ya kuamini safari ya kutinga katika hatua ya robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya ipo mikononi mwao.



Mchezo kati ya Real Madrid dhidi ya Man Utd, utakuwa wa kwanza kwa mshambuliaji huyo kukutana na klabu aliyoitumikia siku za nyuma, na pia mchezo huo utamrejesha kwa mara ya kwanza katika uwanja wa Old Trafford ambao ulikua kama nyumbani kwake kuanzia mwaka 2003–2009 aliposajiliwa akitokea Sporting Clube de Portugal ya nchini kwao Ureno.

 

Wakati huo huo mshambuliaji huyo amepata wakati mgumu wakati akiripoti kwenye kambi ya timu ya taifa ya Ureno, kufuatia baadhi ya mashabiki wa soka nchini humo kumkejeli kwa kumuita jina na Lionel messi ambae kila leo amekua akishindanishwa nae kwenye mijadala ya kimichezo ama kwenye tuzo za kimataifa.



Hata hivyo Ronaldo hakuonyesha kuzijali kelele hizo za baadhi ya mashabikia ambao walionekana kuwa na lengo la kumkejeli baada ya kushindwa na mshambuliaji huyo kutoka nchini Argentina kwenye ushindani wa tuzo ya mchezaji bora wa dunia.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger