Pages


Home » » TAIFA STARS na CAMEROON kuumana leo moja kwa moja Jijini Dar es salaam...

TAIFA STARS na CAMEROON kuumana leo moja kwa moja Jijini Dar es salaam...

Kamanga na Matukio | 03:11 | 0 comments

Ngassa(Pichani) akiwa mazoezini wakati, Kikosi cha Taifa Stars kikifanya mazoezi ya mwisho kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Cameroon utakaofanyika leo uwanja wa Taifa jijini Dar
 
Timu ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS, leo itacheza mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya waliokua mabingwa wa barani Afrika mwaka 1984, 1988, 2000 pamoja na 2002 timu ya taifa ya Cameroon.


Mchezo huo unatarajia kuanza majira ya saa kumi na mkoja jioni katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam, unasubhiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka hapa nchini pamoja na sehemu nyingine za barani Afrika kufutia mwenendo mzuri wa Taifa Stars ambao walifanikiwa kuwafunga mabingwa wa Afrika mwaka 2012 timu ya taifa ya zamabia mwishoni mwa mwaka jana.


Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania Kim Poulsen amesema mchezo huo utakua na umuhimu mkubwa kwa kikosi chake ambacho mwezi ujao kitakabiliwa na mchezo wa kufuzu katika fainali za kombe la dunia za mwaka 2014 dhidi ya timu ya taifa ya morocco.


Kim Paoulsen amesema kikosi chake kipo kamili baada ya kukusanyika kwa wakati, na pia kipo tayari kuwaikabili timu ya taifa ya Cameroon katika mchezo wa leo, huku akisisitiza neno umoja ni nguvu kama chagizo la mafanikio katika mpambano huo



Kwa upande wa nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS Juma Kasseja Juma amesema anaamini maandaliozi waliyoyafanya kwa siku mbili yanakidhi kupambana na kikosi cha Camaroon ambapo hata hivyo amekiri bado mchezo utakua mgumu baina ya pande zote mbili.



Wakati huo huo kocha mkuu wa timu ya taifa ya Cameroon Jean Paul Akono amesema mchezo wa leo upo wazi kwa kila mmoja kuchomoza na ushindi kutokana na viwango vya soka barani Afrika kubadilika kutokana na mazingira ya ushindani yaliopo kwa sasa.


Akitafsiri yaliyosemwa na kocha huyo kutoka lugha ya kifaransa, meneja wa The Indomitable Lions Rigobert Song mbae aliwahi kuwa nahodha wa kikosi cha Cameroon amesema  wamekuja nchini kusaka namna ya kujiaandaa ipasavyo kutokana na uwezo wa timu ya Tanzania kupanda kwa haraka.



Katika hatua nyingine serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kup[itia wizara ya habari, vijana utamaduni na michezo imeitakia kila la kheri Taifa Stars katika mchezo huo muhimu wa kujiandaa na michuano kabambe inayowakabili kwa ajili ya kupata nafasi ya kushiriki kwenye fainali kubwa dunia.


Waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo Fenella Mukangala amesema wapo nyuma ya timu hiyo kwa kila hali na wanaamini kocha mkuu amekiandaa vyema kikosi chake kwa ajili ya kupata ushindi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger