Pages


Home » » Mama aliyemlisha Kinyesi na kumchoma moto mtoto ahukumiwa kifungo cha maisha jela.

Mama aliyemlisha Kinyesi na kumchoma moto mtoto ahukumiwa kifungo cha maisha jela.

Kamanga na Matukio | 17:44 | 0 comments
Wilvina Mkandala (24) akitolewa mahakamani mara tu baada ya kusomewa hukumu ya kifungo cha maisaha 
Baadhi ya wakazi wa majengo alikokuwa anaishi mtuhumiwa wakimsifu hakimu kwa hukumu aliyotoa kwa mtuhumiwa huyo
Mtoto Aneth kabla ya kukatwa kwa mkono wake wa kushoto
Mtoto Aneth mara baada ya kukatwa mkono wa kushoto kwa ujumla mtoto huyu anaendelea vizuri na alishatoka hospitalini.


Na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
WILIVINA MKANDALA mwenye umri wa miaka 24 ameukumiwa kutumikia kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na hatia ya kumlisha mtoto ANETH GASTO mwenye umri wa 5 mitano kinyesi na na kumuunguza kwa maji ya moto

Akisoma hati ya mashtaka mwendesha mashtaka wa serikali ACHIREY MULISA ameiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa watu wegine wenye tabia kama hiyo

Akisoma hukumu hiyo kwa muda wa dakika hamsini hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya mbeya GILBERT NDEURUO ameridhishwa na   na ushahidi uliotolewa na upande  wa Jamuhuri kwamba  mshtakiwa amtenda kosa kinyume cha sheria  cha makosa ya jinai namba 222(a)sura  ya kumi na sita ya marekebisho ya mwaka 2002

Hata hivyo ameiomba serikali kutunga sheria ya kumlinda  mtoto kutokana na vitendo vilivyokithiri kwa  watoto ambapo amesema tanzania haina sheria ya kulinda mtoto

Akijitetea mahakamani mtuhumiwa huyo   ameiomba mahakama kumpunguzia adhabu kwani anategemewa na familia sababu ambazo zilipingwa na mahakama hiyo
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger