Pages


Home » » RC MBEYA AWAONYA WANAOANZISHA VYUO VYA UFUNDI STADI KIENYEJI

RC MBEYA AWAONYA WANAOANZISHA VYUO VYA UFUNDI STADI KIENYEJI

Kamanga na Matukio | 02:29 | 0 comments
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mh Abbas Kandoro.
 Na Esther Macha, Mbeya
MKUU wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abbas Kandoro ameonya tabia ya baadhi ya watu ambao wamekuwa wakianzisha vyuo  vya Ufundi Stadi kienyeji bila ya kuwa na usajili wowote kutoka serikalini hali ambayo imekuwa ikirudisha nyuma  maendeleo ya elimu ya ufundi nchini.

Amesema kuwa vyuo vingi vya ufundi vimekuwa vikianzishwa tu bila kufuata utaratibu wowote na wahusika na hivyo kusababisha wanafunzi kukosa sifa za kufanya mtihani yao ya mwisho.

Bw. Kandoro aliyasema hayo jana wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wamiliki wa Vyuo vya ufundi stadi,pamoja na wakuu wa  vyuo vya ufundi stadi na secretariat ya Veta Kanda ambapo mafunzo hayo yanafanyika katika ukumbi wa mikutao wa veta uliopo chuoni hapo.

“Hali hii inasikitisha sana ukitembea mitaani huko vyuo vimejazana lakini havina usajili na kwamba hali hiyo inapoteza muda sana kwa vijana wetu  kwani baadaye huambiwa hawana namba za usajili wakati wa kufanya ,mitihani yao ya mwisho kutokana na kutokuwa na namba za usajili ambazo zinasababisha vyuo hivyo kuendeshwa bila kufuata utaratibu na sheria”alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Hata hivyo alisema kuwa kama mkoa hawana tatizo na watu ambao wanaanzisha vyuo kwani lengo lao ni zuri la kuhakikisha kuwa kila kijana anapata ajira badala ya kukaa vijiweni,kikubwa  ni kufuata taratibu za serikali ili kuwa na usajili halali.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema vyuo vikiwa vingi vitasaidia vijana kuwa na elimu ambayo ni endelevu na kwamba kupitia ufundi huo vijana wanazpata ujuzi wa ufrundi mbali mbali.

Aidha Bw. Kandoro aliwashauri wazazi na vijana  kuona kuwa elimu ya ufundi  stadi ni mchepuo mwingine wa elimu na sio chaguo la mwisho mara wanapokosa  fursa  ya kuendelea  na elimu ya sekondari  au elimu ya juu.

Alisema wazazi wana wajibu kuweka kipaumbele elimu ya ufundi kwani ni sawa na elimu nyingine ambazo zimekuwa zikipewa nafasi .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Veta Kanda ya Kusini Magharibi Bw.Justine Rutta alisema maqfunzo hayo yatajumuisha washiriki kutoka mikoa ya , Mbeya, Rukwa pamoja na Kata na kwamba mkutano huo utakuwa na washiriki 64 ambao utakuwa na wamiliki  wa vyuo vya ufundi stadi,wadau mbali mbali wa elimu   na mafunzo ya ufundi ,wakuu wa vyuo vya ufundi stadi.

Bw. Rutta alisema kuwa katikia mafunzo hayo kila chuo kitasoma taarifa fupi ya chuo chake ili kufahamu mapungufu yaliyopo ,pamoja na  miongozo na taratibu za usajili wa vyuo ili kuwa na vyuo vya ufundi stadi vyenye hadhi  bora.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger