Pages


Home » » MAKUNDI YALIYOGAWANYIKA NDANI YA CCM NI CHANZO CHA KUPOTEZA VITI VYA UBUNGE

MAKUNDI YALIYOGAWANYIKA NDANI YA CCM NI CHANZO CHA KUPOTEZA VITI VYA UBUNGE

Kamanga na Matukio | 02:26 | 0 comments
Na Ester Macha,
NAIBU waziri wa  Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw.Adam Malima amesema kuwa sababu kubwa ambayo inayochangia kupoteza viti vya ubunge katika maeneo mbalimbali nchini ni kutokana na makundi yaliyogawanyika ndani ya chama kipindi cha kura za maoni ndani ya chama hicho.

Amesema kuwa makosa ambayo huwa yanafanyika wakati wa kupitisha majina ambapo jina linalopitishwa linakuwa sio chaguo la wanachama  hivyo hulazimika kumpa mtu yeyote kutokana na chama kuweka jina ambalo halitakiwi kwa wanachama.

Bw. Malima alisema yote inatokana  na chama cha mapinduzi kupoteza viti vya ubunge katika maeneo mbali mbali ni kutokana wagombea walio wengi kukataliwa kwenye kura za maoni ndani ya chama hicho.

Akitolea mfano Mkoa wa Iringa alisema kwamba Mbunge wa sasa Mchungaji Msigwa hana uwezo wa kuwa Mbunge katika jimbo la Iringa bali wananchi walilazimika kumchagua kutokana na kura za maoni  ndani ya ccm katika kumchakato wa kumchagua mgombea wa Ubunge wa jimbo hilo..

Bw. Malima alisema hayo jana wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa uchaguzi wa chama cha mapinduzi uliofanyika katika viwanja vya sokoine Jijini hapa.
 
“Mfano tosha tunao kutoka Mkoa wa Iringa jina lililopitishwa ndani ya halmashauri kuu ya CCM  halikuwa chaguo la wanachama  hivyo wananchi wote wakalazimika kumchagua Mbunge ambaye hakupaswa kuwa mbunge “alisema Bw. malima.

Akizungumzia kwa Mkoa wa Mbeya alisema kuwa kwamba kwa kawaida Mbeya ni ya chama cha mapinduzi lakini katika uchaguzi uliopita walijikwaa ndio maana ilifika mahala wakapoteza viti viwili  vya ubunge ambavyo ni Mbeya Mjini na Mbozi Magharibi.

Alisema kuwa hata Mbunge wa jimbo la Mbeya mjini Bw.Mbilinyi nae hana uwezo wa kuingia bungeni na kuwatetea wananchi wake hali kadhalika na Mbozi magharibi pia hawafanani na wananchi wanaowaongoza ambao wanatakiwa kwenda kuwatetea bungeni bali yote hiyo ilitokana na kujikwaa kwa chama .

Hata hivyo alisema kwamba katika chaguzi mbali mbali ndani ya chama cha mapinduzi ni sawa na usajili wa timu ambayo itakayokwenda kushindana mwaka 2015 hivyo makosa yaliyofanyika kipindi kilichopita inatakiwa kuyarekebisha sasa  ili kuondokana na makundi yasiyokuwa na tija ndani ya chama cha mapinduzi ambayo yamekuwa yakitoa nafasi ya kushinda kwa vyama vya upinzani .

“Uchaguzi huu ambao tunafanya leo ni usajili wa timu itakayokwenda kushindana kwenye uchaguzi wa mwaka 2015 hivyo ni vema tukawa na timu nzuri ambayo itakuwa na nguvu kubwa na upinzani kushindwa kutumia mianya hiyo ambayo imekuwa ikitoa nafasi  kubwa kwa wapinzani kupenye kwa kutumia makundi yetu ndani ya chama”alisema Malima.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger