Pages


Home » » TAASISI ZA SERIKALI ZAONGOZA KWA MADENI

TAASISI ZA SERIKALI ZAONGOZA KWA MADENI

Kamanga na Matukio | 02:50 | 0 comments
Na Ester Macha,Mbeya.
MAMLAKA ya majisafi na Usafi wa Mazingira Jiji la Mbeya, imesema  kuwa  shule za serikali pamoja na  jeshi la polisi  ndizo zinaongoza kwa  kuwa na madeni ya makubwa ya maji kutokana na kutolipwa kwa wakati na hivyo kusababisha mamlaka kuwa na utendaji mgumu wa kazi .

Kufuatia kuwepo kwa madeni hayo  mamlaka  ya maji imeanza opareshemni ya kukata maji kwa maeneo yote ya wananchi ambako hawajalipa ada.

Kauli hiyo imetolewa jana na Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya maji Jijini hapa Bibi. Neema Stanton wakati alipozungumza na gazeti hili ofisini kwake kuhusu  ulipaji wa madeni ya maji kwa taasisi za serikali ,makampuni binafsi pamoja na wananchi.

“Kwenye huu ulipaji wa madeni ya maji kwakweli hizi taasisi za serikali zimekuwa ni tatizo kubwa kwa upande wa madeni  licha ya kuwa mamlaka bado inaendelea na jitihada za kuhakikisha kuwa madeni hayo yanalipwa mapema”alisema.

Akizungumzia kwa upande wa shule za sekondari za serikali Bi.Stanton alisema nazo zimekuwa zikisuasua  kwa kiasi Fulani  kutokana na wao kuweka kipaumbele mambo Fulani kwenye  shule zao.

Hata hivyo Ofisa Uhusiano huyo alisema  kwa upande wa shule  za sekondari za binafsi  wao wamekuwa wepesi wa kulipa  madeni  lakini kwa kufuatiliwa sana  na mamlaka ndipo wanalipa  madeni hayo.

“Lakini pia licha ya kuwa  wanalipa lakini ni wajibu wao kutakiwa kulipa kwa wakati  bila kufuatwa kwani kulipa ni wajibu wao sababu wanatumia maji isitoshe kwa suala la shule ambalo ni muhimu zaidi”alisema.

Aidha Bibi.Stanton alitoa wito kwa shule za serikali  kuweka kipaumbele  ulipaji wa bili za maji  kwani fedha hizo zinasaidia malipo ya umeme,madawa kwenye maji ambayo yanatumia grama kubwa.

“Kwa ujumla grama za uendeshaji ni  nyingi  hivyo ni vema shule na taasisi za serikali zikatambua  umuhimu wa huo “alisema.

Hata hivyo Ofisa uhusiano huyo alipotakiwa kuzungumzia kiasi kamili cha madeni ambayo mamlaka ya maji inadai alisema suala hilo lipo kwa meneja ambaye ndiye ana  takwimu sahihi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger