Pages


Home » » WATU 14 WAFUTIWA MASHTAKA YA KOSA LA JINAI.

WATU 14 WAFUTIWA MASHTAKA YA KOSA LA JINAI.

Kamanga na Matukio | 05:18 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbozi.
Bwana Paulo Sichone na wenzake 13 wote Wakazi wa Kijiji cha Myunga, Kata ya Myunga, Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya wamefutiwa mashtaka  wamejikuta wakibubujikwa na machozi ya furaha baada ya kuachiwa huru na mahakama ya wilaya ya Mbozi mkoani hapo Oktoba 2 mwaka huu.

 Watu hao walikuwa wakikabiliwa na kesi namba 143/2012, wakituhumiwa kwa kosa la kutumia silaha na unyang'anyi ambapo kwa pamoja wanadaiwa kuvunja nyumba ya Bwana Benard Simundwe na kuiba mali zenye thamani ya shilingi milioni 87, kinyume cha sheria ya makosa ya jinai kifungu cha 287(a).

"Kwa pamoja mheshimiwa naiomba mahakama yako Tukufu kuwaachia huru washtakiwa wote, kwa kutumia Kifungu cha 91 cha sheria na Jamhuri haina nia ya kuendelea na kesi hiyo" alisema muendesha mashtaka mahakamani hapo.

Baada ya kauli hiyo ya mwendesha mashtaka, Wakili wa washtakiwa mheshimiwa Edgar Bantulaki alikubaliana na mwendesha mashtaka, hivyo wateja wake kuwa huru kuanzia Oktoba 25 mwaka huu tangu walipokamatwa Agosti 13 mwaka huu na wengi wao kudhalilishwa na Jeshi la Polisi wakati wa operatioh hiyo.

Aidha baada ya kesi hiyo kumalizika mahakamani washtakiwa hao walilakiwa na ndugu zao wakiongezwa na Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Satiel Japhet Sikanyika na Diwani wa kata ya Iyunga Bwana mheshimiwa Godfrey Siame ambao kwa pamoja wamesema wanamshukuru Mungu kwa shari lao kumalizika kwani shughuli za uchumi zilizorota kijijini hapo kwani muda mwingi walikuwa wakiutumia kuhudhuria kesi ya mahakamani na gharama kubwa za nauli kutoka Myumba.

Kwa upande wake nje ya mahakama wakili Edgar aliwataka wananchi hao kutokuwa na risasi hivyo wasamehe na kupotezea kabisa hivyo wasamehe na kusahau yote yaliyopita.

Pia Mcungaji wa Kanisa la Moravian Tanazania, Jimbo la kusini Magharibi, Mchungaji Isaya Simsokwe amewaambia wananchi wa Kijiji cha Myunga kumtegemea Mungu wakati wao ndio maana ametetea na kuwashindia katika kesi hiyo nzito ambayo imesababisha wengine kuuza Chakula ili kukabiliana na keshi hiyo.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida mlalamikaji katika kesi hiyo Bwana Benard Simunde, alionekana mahakamani hapo hali inayotia shaka utendaji wa Jeshi la Polisi kwa kufadhili mtandao wa uhalifu, licha ya kukabiliwa na kuhusika na vitendo vya mauaji lakini Polisi wamekuwa wakimwangalia bila kuchukua hatua zozote na wakati meingine kunywa nae juice kama ilivyokuwa imetokea Oktoba 25  Bwana Simundwe alipokuwa  na askai katika mgahawa uliopo Posta eneo la Kiwila Mbozi.

Hata hivyo vielelezp vilivyowasilishwa kituo cha Tunduma na Mbozi vimetoweka katika hali ya Tunduma na Mbozi vimetoweka katika hali ya kutatanisha ilinayompa wakati mgumu Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mbeya Diwani Athumani vilivyodhibiti vitendo vya rushwa vilivyokithiri katika vituo mbalimbali .
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger