Pages


Home » » WATU WAWILI WAJERUHIWA KWA RISASI KATIKA VURUGU - CHUNYA.

WATU WAWILI WAJERUHIWA KWA RISASI KATIKA VURUGU - CHUNYA.

Kamanga na Matukio | 05:11 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga, Chunya.
Wakazi wawili wa Kijiji cha Iyovyo, Kata ya Totowe, Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wamejeruhiwa kwa risasi kufuatia vurugu kuzuka kijijini hapo mnamo Oktoba 7 mwaka huu majira ya saa 12 jioni.

Diwani wa Kata ya Totowe mheshimiwa Godian Wangala, amewataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na Bi, Asha Juma(31) na Bwana Yasin Damisiano Nambuyu(44) ambalo walijeruhiwa vibaya na Askali waliokuwa na silaha kwa lengo la kumkamata mhalifu Zunzu Sengeka(38), anayetuhumiwa kubaka na kulisha mifugo katika mashamba kadhaa katika Kitongoji cha Maleza hivi karibuni.

Mtuhumiwa huyo na wenzake 9 walimbaka mke wa mkulima kijijini hapo baada ya kumfungia mumewe katika nyumba yake na kumjeruhi vibaya na kutokomea kusikojulikana, lakini baada ya ukatili huo kutendeka mwanamke alikimbizwa katika Zahanati ya Mkwajuni na taarifa kutolewa Kituo cha Polisi cha Galula wilaya hiyohiyo.

Aidha, baada ya taarifa hizo Jeshi la polisi wakiwa na pikipiki walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa Bwana Sengeka ndani ya kijiji hicho hicho na kisha kumfunga pingu na kumpakia katika pikipiki hiyo na walipojaribu kuondoka mtuhumiwa alifanya vurugu na kusababisha pikipiki kuanguka ndipo kundi la wafugaji wakiwa na silaha mbalimbali za jadi na fimbo walianza kuwashambulia askari hao.

Hali hiyo iliwalazimu Askari kufyatua risasi kwa ajili ya kuwatawanya wananchi hao ndipo ziliwajeruhi Bi Asha na Bwana Nambuyu miguuni na kukimbizwa Kituo cha Afya cha Mkwajuni ambapo hali zao kwa sasa wanaendelea vema baada ya kufika kituoni hapo kutokana na juhudi kubwa za Diwani kwa kutumia pikipiki mbili majira ya saa saba usiku Oktoba 8 mwaka huu.

Hata hivyo Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutoa onyo kwa wananchi kutojichukulia sheria mikononi na kuahidi kuwa wale wote waluiohusika na tukio hilo watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. Mgogoro wa wakulima na wafugaji umedumu kwa muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger