Pages


Home » » MAHAKAMA YA WILAYA YA MBOZI LAWAMANI KWA KUCHELEWESHA KESI.

MAHAKAMA YA WILAYA YA MBOZI LAWAMANI KWA KUCHELEWESHA KESI.

Kamanga na Matukio | 03:41 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Kitendawili cha hatima ya kesi namba 143/2012 kimeshindwa kuteguliwa na Hakimu wa Mahakama ya wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya baada ya kesi hiyo kuahirishwa hadi Oktoba 25 mwaka huu baada ya Oktoba 18,mahakama hiyo kushindwa kutoa maamuzi kama ilivyoahidi  Oktoba 15 mwaka huu.

Kesi hiyo inayomhusu Bwana Paulo Sichone na wenzake 12 ilikuwa itolewe maamuzi Oktoba 18 mwaka huu lakini jalada la kesi hiyo kudaiwa kuwa halipo mahakamani kwa mujibu wa maelezo ya Mwendesha Mashtaka.

Oktoba 18 mwaka huu, Mwendesha Mashtaka ameiambia mahakama hiyo kuwa jalada hilo limepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali mkoani hapa, hali iliyopelekea washtakiwa kuendelea kusota mahabusu baada ya mwendesha mashtaka kukataa dhamana.

Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida Jeshi la Polisi limemwachia kwa dhamana Bwana Benard Simundwe, anayedaiwa kujihusisha na mtandao wa majambazi licha ya vielelezo kuwasilishwa Polisi Kituo cha Tunduma na Mbozi na Polisi kudai kuwa havipo hali iliyozua maswali mengi kwa wapenda haki na amani tukio lilitohusishwa na kuwepo kwa Rushwa ndani yake na kuthibitisha kuwa mwenye pesa siyo mwenzako kutokana na wanyonge kusota mahabudu huku wenye pesa wakitanua mitaani.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger