Pages


Home » » WATAKA SUMATRA,POLISI KUKAGUA MABASI MABOVU

WATAKA SUMATRA,POLISI KUKAGUA MABASI MABOVU

Kamanga na Matukio | 02:51 | 0 comments
Hawa Mathias,Mbeya.
BAADHI ya wananchi  wanaotumia vyombo vya usafiri maarufu (daladala) Mkoani Mbeya  wameomba mamlaka ya usafirishaji wa nchi kavu na majini (SUMATRA)  kushirikiana na jeshi la polisi kufanya ukaguzi    wa  haraka   wa magari mabovu ili kuweza  kuthibiti ajari za barabarani  zinazochangiwa na ubovu wa vyombo vya usafiri.

 Wakizungumza na  Mwananchi  baadhi ya wananchi wanaosafiri kati   Sokomatola kwenda  uyole  na sokomatola Mbarizi wamesema kuwa vyombo vingi  vya usafiri   havina sifa ya kusafirisha abiria na badala yake wamiliki wamekuwa wakitanguliza maslai ya fedha badala ya uhai wa abiria na mali zao.

"Ifikie wakati idara husika kusimamia hilo na kusikiliza kero za wananchi na  na kuwataka  askari wa jeshi la polisi kitengo cha usalma barabarani kutojenga mazoea na madereva na makondakta  na badala yake wafanye kazi kwa kuzingatia maadili na kanuni za kisdheria ili kukabiliana na hali hiyo ili kuthibi hali ya usalama barabarani "Alisema Jordan Mwaisanila mkazi wa uyole

"Tunaomba  sumatra kushirikiana na jeshi la polisi na umoja wa chama cha madereva ili kuweza kukaa pamoja na kujua nini cha kufanya ili kuthibiti hali hii kwani mabasi mengi ni mabovu na madereva wengi wamekuwa wakikiuka sheria za usalama barabarani kwa kuendesha magari kwa mwendo kasi,kutovaa sare na kutoa lugha chafu kwa abiria"Walisema.

Naye Mkazi wa Mji mdogo wa mbarizi Selina Jonhson alisema kuwa sasa ifikie wakati jeshi la polisi kitengo cha usalama barabani kuweka mikakati kabambe ili kuhakikisha linaendesha zoezi  kwa kuzingatia kanuni na sheria na kutomuonea  kwa kutoza faini kubwa  ili kuweza kutoa fundisho kwa  wamiliki wa vyombo vya usafiri waweze kutambua wajibu wao wa kuvifanyia matengenezo vyombo vya usafiri na si kutanguliza masli ya fedha mbele.

"Sasa ifikie wakati hata polisi wa usalama barabarani akufanya ukaguzi wa magari na kufanya mazoea na madereva na makondakta na hivyo ni jukumu lenu kutambua nini kinachowaweka barabarani kwani kukagua leseni na mataili bado hamjatambua ubovu wa vyombo vya usafiri"Alisema Jordan Mwasakyeni.

Johnson alisema kuwa wamiliki wa  vyombo vya usalama wanapaswa kutambua majukumu yao kwa watazania  kwa  kufanya  ukarabati na matengenezo  ili kuepuka hasara na vifo vya wananchi vinavyotokana na ajari za barabarani.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger