Pages


Home » » WAKULIMA NA WAFUGAJI WATOLEANA UVIVU - WILAYANI MBARALI.

WAKULIMA NA WAFUGAJI WATOLEANA UVIVU - WILAYANI MBARALI.

Kamanga na Matukio | 05:21 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
*Mwananchi mmoja achomwa mkuki,Polisi wakimbia.
Ugomvi baina ya Wafugaji wa Wakulima umezuka katika Kijiji cha Simike - Utengule Usangu, Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya na kusababisha mwananchi mmoja anayefahamika kwa jina Abeli Mwakyoma kujeruhiwa baada ya kuchomwa mkuki na kundi la wafugaji wa jamii ya Kisukuma.

Wananchi watatu wanaofahamika kwa jina la Bi. Magreth Simwela, John Kayange na Richard Mwasyanga walinusurika kupigwa na kundi la wafugaji waliokuwa na kundi la ng'ombe, hali iliyopelekea kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha Igurusi.

Aidha Polisi wa kituo hicho walifanikiwa kuwakamata Juma Mwambeta, Daniel Edward, Stephen, Walusungo Vaisi na Vedasto Simwaba wakidaiwa kuwafungulia ng'ombe kutoka zizini na mara baada ya kupata taarifa, Polisi walilazimika kwenda eneo la tukio na kukuta kundi jingile la ng'ombe likila mazao shambani.

Baada ya ng'ombe kukusanywa mifugo hiyo kundi la wafugaji lilianza kuwashambulia Askari na wakulima kwa kutumia silaha za fimbo na mikuki, hali iliyopelekea Polisi hao kukimbia..

Kupitia sakata hilo wafugaji walifanikiwa kumkamata Bwana Abeli Mwakyoma na kuanza kumshambulia na alipofanikiwa kukimbia alichomwa mkuki kiunoni na baada ya umbali kadhaa aliomba msaada wa kunasuliwa mkuki huo na kukimbizwa katika Hispitali ya Chimala Mission,ambapo alilazwa na kuruhusiwa Oktoba 9 mwaka huu baada ya kupatiwa huduma ya matibabu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger