Pages


Home » » WAKUNGA WA JADI WAZALISHA WANAWAKE WAJAWAZITO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU - CHUNYA,

WAKUNGA WA JADI WAZALISHA WANAWAKE WAJAWAZITO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU - CHUNYA,

Kamanga na Matukio | 05:35 | 0 comments
Na Ezekiel Kamanga, Chunya.
Wakunga wa jadi wawili wanaofanya shughuli ya kuwazalisha wanawake wajawazito katika Kata ya Totowe,Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wamewaokoa wanawake wengi,licha ya kukabiliwa  na Chnamoto mbalimbali katika ufanikishaji wa fani hiyo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa vitendea kazi.

Mmoja wa wakungunga anayefahamika kwa jina la Bi.Hilda Said Kawinga(80),amesema mpaka sasa amewazalisha wajawazito 55 mwaka huu na walipokelewa kwake siku mojakbalya yakujifungua na hakuna kifo chochote kilichowahi kutokea  na kuorodhesha katika Daftari  lake na ilimlazimu kufanya hivyo ili kuisaidia Serikali kupata takwimu endapo zitahitajika,

Amesema kuma kuwa changamoto aliyonayo ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya studio kama vile mkasi,vyombo vya kuhifadhia maji,kitanda na godoro ambapo amesema kwa wastani hupokea zawadi ya wajawazito 10 kwa mwezi na hakuna tozo kwa huduma hiyo mara baada ya kujifungua.

Kwa upande wake Mkunga mwingine Bi, Agripina Fredrtick Sikanyika (37) maarufu kama Mama Namwinji,amesema imemlazimu kuwaachia nyumba wagonjwa wanaofika kwa ajili ya kujisubiria kutokana na mfululizo wa wagonjwa hao wanaofika kwake kupata huduma hiyo huku akiacha nyumba nyingine kwa ajili ya kujifungulia.

Mkunga huyo amesema alianza huduma hiyo tangu mwaka 2000 na mwaka 2011 alizalisha wajawazito 114 na mwaka huu wajawazito 187 na kwamba kati ya hao watoto wawili walizaliwa wakiwa na ulemavu wa aina yake.

Mnamo Septemba 15 mwaka huu mwanamke mmoja alijifungua mtoto mwenye sikio moja, mguu mmoja, mdomo na pua vikiwa vimeungana ma mtoto huyo alifariki muda mfupi baada ya kujifungua.

Aidha Septemba 16 mwaka huu pia alizaliwa mtoto aliyekuwa na kichwa mithili ya ng'ombe  na kiwiliwili cha binadamu.

Mbali na matukio hayo mawili ya aina yake,mkunga amesema kuwa yeye hatozi tozo yoyote licha ya kazi ngumu ambayo amekuwa akiifanya usiku na mchana huku ukiwepo uhaba wa kitanda cha kujifungulia wajawazito kwani huwalaza chini na kukabiliwa na magonjwa hasa kipindi cha masika.

Aidha Bi Agripina amesema kuwa hufuata taratibi zote za kuwapokea wajawazito hao kwa kuzikagua kadi za kliniki  na kuzijaza pindi wakijifungua.

Mbali na hilo mkunga huyo pia hupokea wajawazito ambao wanatakiwa kufanyiwa oparesheni/upasuaji na kwake hujifungua salama bila upasuaji wowote na kubainisha kuwa mmoja wa wajawazito alifanyiwa upasuaji kama mara mbili hospitalini lakini alipopelekwa kwake alijifungua watoto wawili salama katika nyakati tofauti.

Hata hivyo Bi Agripina ametoa wito kwa serikali kuwasaidia wakunga kutokana na kufanya kazi hizo ngumu ambazo zingefanywa hospitalini na pia amesikitishwa na kitendo cha Afisa Mtendaji wa Kata ya Mbuyuni kumtoza shilingi laki mbili kwa kile alichodai kuwa ni kifo cha mama mjamzito na stakabadhi ya malipo kutopewa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger