Pages


Home » » WATU WAWILI WAJERUHIWA NA SIMBA - MBOZI.

WATU WAWILI WAJERUHIWA NA SIMBA - MBOZI.

Kamanga na Matukio | 06:03 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Watu wawili waishio Kijiji cha Shasya,Kata ya Halungu,Wilaya ya Mbozi Mkoania Mbeya wamenusurika kifo baada ya kujeruhiwa vibaya na mnyama anayedhaniwa kuwa simba kijijini hapo.

Akizungumzia tukio hilo Diwani wa Kata ya Halungu mheshimiwa Samson Simkoko,amewataja waliojeruhiwa ambao wamefahamika kwa jina moja ni pamoja na Nzowa na Simkoko,tukio lililotokea katika msitu wa Shasya wakiwa katika shunguli ya kuwinda Nguruwe Pori mnamo Agosti 6 mwaka huu.

Katika sakata hilo Simba huyo alianza kuwashambulia na katika mapambano hayo watu hao wamejeruhiwa vibaya,licha ya kujikongoja hadi kijijini na kuomba msaada na kukimbizwa katika Hospitali ya Mbozi Mission,ambapo hali zao zimetajwa kuendelea vema.

Aidha Diwani Simkoko alitoa taarifa katika Kituo cha Polisi Halungu,na majeruhi kupewa PF3 kwa ajili ya matibabu na kisha alitoa taarifa katika Ofisi ya Maliasili,Wilaya ya Mbozi na sasa wanafanya msako mkali kwa kushirikiana na wananchi kumsana Simba huyo.

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger