Pages


Home » » CHADEMA WAENDELEA KUJIZOLEA WANACHAMA WAPYA.

CHADEMA WAENDELEA KUJIZOLEA WANACHAMA WAPYA.

Kamanga na Matukio | 03:40 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbarali.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA),kimeendelea kujizolea wanachama wapya baada ya kufanya mkutano wa hadhara Agosti 8 mwaka huu katika Kijiji cha Kongoro Mswisi,Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya.

Mkutano huo ulifunguliwa na Mwenyekiti wa chama hicho wilaya Bwana Peter Mwashite wakiwa na nia ya kutoa shukrani kwa wananchi wa kijiji hicho waliokipigia kura chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2010 wa kuchangua Rais,Wabunge na Madiwani,licha ya kura kutotosha kukiwezesha chama hicho kuibuka na ushindi.

Aidha,katika mkutano huo viongozi kadhaa wa chama hicho walipanda jukwaani na kunadi sera za chama akiwemo aliyewahi kugombea nafasi ya ubunge wa Jimbo la Mbarali Bwana Gidawaya Kazamoyo,Diwani wa viti maalumu Lucy Ngonde,Diwani wa Kata ya Kiwira,Wilaya ya Rungwe Bwana Julius Laurent Mwakalibule,Mwenyekiti wa Vijana mkoa Bwana Julius Kasambala na Bi.Agatha John ambaye ni mwenyekiti wa wanawake Wilaya ya Mbeya Mjini.

Katika mkutano huo kadi za wanachama zaidi ya 74 kutokea Chama Cha Mapinduzi(CCM) walijiunga na chama cha CHADEMA.

Akihutubia mkutano huo Diwani wa Viti Maalumu wa wilaya ya Mbarali Bi, Lucy Ngonde,amesema kuwa zaidi ya bilioni 1.4 pesa za Halmashauri ya wilaya hiyo zimefujwa ba kusababisha miradi ya maendeleo kukwama na kwamba pesa hizo ni tofauti ya shilingi milioni 87 zimefujwa na Mweka Hazina wa halmashauri hiyo.

Wakat huohuo amemtaka Mkurugenzi wa wilaya hiyo kutenga bajeti ya fedha kwa ajili ya chaguzi za vitongoji,ambapo imebainika kuwa baadhi ya vijiji vina makaimu wenyeviti kikiwemo Kijiji cha Mswiswi,kitongoji cha Uswafwani hakina mwenyekiti kwa takribani mwezi mmoja mpaka sasa,Majengo Mapya miaka miwili,Mshikamano miaka mitatu na Maendeleo miaka miwili,hali inayopelekea kuzorota kwa maendeleo wilayani humo.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger