Pages


Home » » WADAU WA ELIMU WAIOMBA SERIKALI KUWEKA MJADALA WA KITAIFA JUU YA SHERIA YA ELIMU NA 25 YA MWAKA 1978

WADAU WA ELIMU WAIOMBA SERIKALI KUWEKA MJADALA WA KITAIFA JUU YA SHERIA YA ELIMU NA 25 YA MWAKA 1978

Kamanga na Matukio | 05:46 | 0 comments
Habari na Ester Macha, Ileje.
Wadau wa elimu  wilayani Ileje mkoanii Mbeya wameiomba serikali kuwepo na mjadala wa kitaifa juu ya sheria ya elimu namba 25 ya mwaka 1978  ambayo inadaiwa kutoweka wazi suala la wanafunzi kupeana ujauzito wakiwa shuleni.

Imeelezwa kuwa sheria ya sasa
  iliyopo imekuwa ikitoa adhabu kwa watoto  wa kiume pekee  hivyo wamependeza kuwa kuwa sheria  ambayo wataiuomba kurekebishwa  inapaswa kuwawajibisha wote wawili badala ilivyo hivi sasa,mwanafunzi wa kiume pekee anashitakiwa.

Tatizo la mimba mashuleni
 limeendelea kupamba moto na hivyo kulazimika wadau wa elimu kwa  ushirikiano wa wananchi kuomba  serikali kufanyia  marekebisho sheria ya elimu namba 25 ya mwaka 1978 ili iendane na  wakati uliopo hivi sasa.

Akizungumza wakati wa kikao na wadau wa elimu wilayani hapo Hivi karibuni Mratibu wa Shirika lisilokuwa la kiserikali linalojishughulisha na watoto na akinamama (KIMAWAMBE)Bw. Mohamed Cheto alisema kuwa
  wakuu  wakuu wa shule mbalimbali wilayani Ileje  wameenda  mbalii zaidi na kuhimiza mabadiliko hayo ya sheria ya elimu.

Alisema kuwa kuanzia sasa
 shirika hilo litahakikisha lifanya jitihada za kuhakikisha kuwa tatizo la mimba mashuleni linakuwa ni  historia,kwani ni jambo ambalo limekuwa ni kero kwa muda mrefuna kusababisha watoto wa kike walio wengi kukatisha masomo kwa tatizo la mimba.

Bw.Cheto alisema  watafanya suala la
 elimu kuwa  miongoni mwa wahusika kwa lengo la  kutokomeza  dhana iliyojengeka miongoni mwa jamii hasa wanafunzi wa kike kuwa suluhisho la kumaliza mimba mashuleni na wala sio  kuwashitaki wanafunzi wote mahakamani badala yake ni kukaa meza moja na wahusika  ili kuyamaliza kwa mafunzo na elimu ya saikolojia.

“Hakuna jambo ambalo haliwezekani ila kikubwa ni kujipanga tu kwa kutoa mafunzo  ya elimu ya Saikolojia kwa wahusika wote wawili ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wazazi wa familia zote”alisema.

Hata hivyo wananchi kwa ujumla walisema kuwa kuna haja sheria hiyo  ikafanyiwa marekebisho ili adhabu hiyo iweze kutolewa kwa wote.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger