Pages


Home » » MAKAMPUNI YA UNUNUZI WA ZAO LA PARETO YATAKIWA KUFUATA TARATIBU.

MAKAMPUNI YA UNUNUZI WA ZAO LA PARETO YATAKIWA KUFUATA TARATIBU.

Kamanga na Matukio | 03:08 | 0 comments
Na Ester Macha,Mbeya.
Wamiliki wa makampuni  ya ununuzi  wa zao la pareto Mkoani Mbeya wametakiwa kufuata taratibu zilizowekwa katika ununuzi wa zao hilo ili kuwanufaisha wakulima badala ya kujinufainisha wamiliki pekee.

Mtakwimu wa bodi ya pareto Nyanda za juu kusini ,Tumaini Ngojile amesema ni vema makampuni yanayojishughulisha  na ununuzi wa pareto kufuata taratibu zote zilizowekwa ili kuweza kupata mzazao bora kwa faida ya kulima ambaye kwa kiasi kikubwa ndiye anayeumia.

Ametaja taratibu hizo kuwa ni mnununuzi  kuhakikishe ana leseni ya kazi, lazima anunue pareto inayoletwa kituoni na siyo kwenda majumbani kununua.

Aidha amesema wanunuzi wanatakiwa kutekeleza makubaliano yao kwa kuweka vibao vya majina ya makampuni na bei rasmi za ununuzi kwa siku husika ya soko.

Hata hivyo Ngojile amehimiza mizani zinazotumika zikaguliwe kabla ya kwenda kufanyia kazi ili kuepuka udanganyifu unaweza kufanywa na wanunuzi,alipiga maarufuku kununua pareto mbichi kwani inalenga kuzooretesha ubora wa zao hilo.

Aidha ametoa wito kwa wakulima na makampuni, wakulima wasikubali kuuza pareto kwa walanguzi kwani lengo lao siyo la kibiashara na badala yake wanalenga kuzoretesha zao  hilo  na kwamba makampuni yatakayobainika yanalangua na kununua pareto majumbani sheria kali zinachukuliwa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger