Pages


Home » » UCHAMBUZI. IMANI POTOFU KWENYE MATUMIZI YA SARAFU KWENYE POMBE ZA KIENYEJI

UCHAMBUZI. IMANI POTOFU KWENYE MATUMIZI YA SARAFU KWENYE POMBE ZA KIENYEJI

Kamanga na Matukio | 05:48 | 0 comments
Na Ester Macha.
Katika kuhakikisha kuwa kila mwananchi anaweza kuendesha maisha yake ya na familia wananchi wamekuwa wakijitahidi kubuni mbinu mbadala za biashara ili waweze kujikwamua kiuchumi ili waweze kuondokana  na hali duni ya kimaisha .

Kundi ambalo limekuwa likijikita zaidi katika harakati za kuendesha maisha wanawake waliopo vijijini na mijini ambao asilimia kubwa wamekuwa walezi wa familia zao.

Lakini ni ukweli usiopingika kuwa kundi hili la wanawake linahitajitaji msaada wa hali na mali kwa kubuni mbinu zingine ambazo zitaweza kuwasaidia kuliko hili wanalotumia ambalo ni  hatari kwa afya za binadamu.

Hivi karibuni kumeibuka imani potofu kwa wapikaji pombe za kienyeji kutumbukiza sarafu katika mapipa ya pombe  na kuchemsha  kwa pamoja kwa imani kuwa pombe inakuwa kali sana  na hivyo kununuliwa kwa wingi kwa wateja wao.

Kuna umuhimu kwa mamlaka husika kuliona hili kwani linaweza kuleta athari kwa wanywaji bila wapikaji pombe kufahamu hili hivyo  ni vema likafanyiwa utafiti wa kina ili kunusuru afya za wanywaji wa pombe  za
kienyeji.

Biashara hii kwa asilimia kubwa inafanywa na wanawake  na kwamba hali hii inatokana na baadhi ya wanawake kuwa na hali duni ya kimaisha na hivyo kulazimika kubuni mbinu ambayo itawawezesha kuishi maisha yao kila siku.

Lakini  pia ikumbukwe kuwa mbinu ya utumiaji  sarafu katika pombe imewalazimu wanawake walio wengi kutumia njia hiyo kutokana na pombe kutokuwa na uchungu na hivyo kushindwa kununuliwa na wateja ambao wanaamini kuwa ni msaada kwao baada ya kununua kinywaji hicho.

Nionavyo katika utumiaji wa sarafu hizi katika pombe si mzuri kiafya kwani hawa watumiaji wanatumia pasipo kuelewa kuwa kwa binadamu inaleta athari gani hivyo ni muhimu wizara ya afya kuliona hili na  kulifanyia kazi au  kutoa elimu kwa wapikaji wa pombe .

Sawa  sote tunafahamu  ugumu wa maisha  uliopo kwa wananchi lakini kwa mbinu hii ya utumiaji wa sarafu si mzuri hivyo  ni vema wakatafuta njia nyingine ambayo itawawezesha katika upikaji wa pombe hizo kuliko kutumia sarafu ambazo haijulikani zimetengenezwa kwa madini gani.

Njia hiyo kiafya si nzuri nashauri benki kuu ya tanzania kanda ya mbeya kutembelea maeneo ya vijijini na mijini kwa wanawake ambao wanajihusisha na upikaji wa pombe ili kuweza kuwapatia elimu juu ya matumizi ya sarafu katika upikaji wa pombe.

Elimu ikitolewa na kufahamu madhara yake wapikaji wa pombe watakuwa na woga na kubuni biashara nyingine ambayo haitaweza kuathiri afya za wananchi ambao ni nguvu kazi ya taifa inayotegemewa.

Kwa haraka jambo hili linaweza kuwa rahisi lakini lina madhara makubwa hata kama haiwezi kudhuru sasa lakini ni hali ambayo inaweza kutokea baadaye  tena kwa kwa kiwango kikubwa  hivyo ni muhimu likafanyiwa kazi haraka ili kunusuru afya za wanywaji .

Sababu tumezoea serikali huwa inafanyia kazi jambo mpaka pale waone kumetokea athari ikwa jamii lakini hivi hivi jambo hili litachukuliwa kirahisi tu na kuachwa kama lilivyo bila kufanyiwa kazi huku wapikaji wa pombe wakiendelea na shughuli zao ikama kawaida.

Ifike wakati  hata kwa wapikaji wa pombe za kienyeji wafahamu kuwa sarafu si nzuri kwa matumizi ya kinywaji chochote kile ambacho ni matumizi kwa binadamu .

Hata hivyo meneja msaidizi sarafu benki kuu ya tanzania kanda ya mbeya Bw.vincent mtan amewashauri  wapikaji wa pombe za kienyeji  wenye imani potofu ya kutumbukiza sarafu katika mapipa  na kuchemsha kwa pamoja  kwa imani ya kukolea kwa pombe ni uharibifu na makosa kisheria na kwamba jitihada zinaendelea kufanyika kuboresha sarafu.

Alisema kuwa  ili sarafu zisiweze kuchuja rangi  licha ya kuchemshwa kwa muda mrefu katika mapipa ya  pombe huku akisisitiza kuwa sarafu zote kuanzia senti tano  hadi sh.200 bado zipo katika mzunguko na zinatumika kihalali .

Sawa nakubaliana na ushauri wa benki kuu kuwa wananchi waachane na mila potofu lakini hapo naona bado haitoshi ila kitu kikubwa ambacho kinatakiwa kwa wahusika wakuu wa benki kuu na kuwapatia elimu kila kijiji na kata  ili elimu iweze kutolewa kwa kila mwananchi ili waweze kufahamu madhara ya utumiaji wa sarafu.

Lakini pia ikumbukwe kuwa  imani hiyo potofu kwa wananchi juu ya matumizi ya sarafu  katika upikaji wa pombe  unatokana na ugumu wa maisha uliopo katika jamii na hivyo katika kujitahidi kujinasua kimaisha wananchi wameona mbinu bora  ambayo itaweza kumudu maisha yao ni kutumia sarafu katika pombe ili iweze kuwa kali na hatimaye kupata wateja kwa wingi.

Nionavyo watendaji  wa kata na wenyeviti wa mitaa waanze zoezi hili mapema kwa kupita katika nyumba ambazo wananchi wake wanapika pombe za kienyeji kuchunguza kwa undani zaidi ili kubaini matumizi hayo ya sarafu katika pombe za kienyeji.

Hii itaweza kusaidia kwa kiasi fulani na kubaini wananchi ambao wanatumia sarafu hizo lakini ili zoezi hilo liweze kwenda vizuri hakuna budi wakaenda nalo taratibu .

Pia elimu hiyo itumike hata kwa wale ambao hawajihusishi na upikaji wa pombe kwa kuitisha mikutano ya hadhara katika vilabu vya pombe za kienyeji maana huko ndiko wanywaji wengi walipo,

Jukumu hili pia linapaswa kuanzia ngazi ya vijiji na kata na mjini kwani ni hali ambayo itaanza kuleta athari kubwa kwa jamii hivyo ni vema mamlaka zinazohusika kuzingatia  na kulifanyia kazi mapema ili kunusuru afya za watumiaji wa pombe za kienyeji.

Lakini ni vizuri pia serikali nayo mikajitahidi kukaa na wananchi wake kuhimiza kufanya miradi mingine ya kimaendeleo ambayo itakuwa haina madhara kwa wananchi na ambayo itakuwa na tija kwa wananchi kuwawezesha kumudu maisha yao ya kila siku.

Kwani yote hii inatokana na viongozi husika wa mitaa na kata kutokuwa wabunifu wa wa miradi kwa wananchi wake kwa kuanzisha miradi mbali mbali ambayo haina madhara kwa binadamu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger