Pages


Home » » Mwanafunzi afikwa na mauti baada ya kunywa sumu, Ajali ya Barabara yaua Mkoani Mbeya

Mwanafunzi afikwa na mauti baada ya kunywa sumu, Ajali ya Barabara yaua Mkoani Mbeya

Kamanga na Matukio | 05:44 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Watu wawili wamefariki dunia Mkoani Mbeya katika matukio mawili likiwemo la mwanafunzi kunywa sumu inayosadikika kuwa ni sumu ya panya,baada ya kufokewa na Bibi yake kwa kosa la kuchelewa kurudi nyumbani.

Tukio hilo limetokea Agosti 18 mwaka huu majira ya saa mbili usiku Shukrani Ndembo(18) mwanafunzi wa Kidato cha Tatu katika Shule ya Sekondari Isange na Mkazi wa Kitongoji cha Ndamba,Kijiji cha Isange,Wilayani Rungwe amejikuta akipoteza uhai wake baada ya kunya sumu hiyo.

Sakata hilo lilianzia pale Bibi wa marehemu alipomtuma binti huyo dukani kununua mahitaji na kisha kuchelewa kurudi nyumbani na baada ya kuulizwa marehemu aliamua kuchukua sumu na kuinywa,ambapo hali yake ilikuwa mbaya na juhudi za kumkimbiza hospitalini zilifanyika lakini ziligonga ukuta baada ya marehemu kufikwa na mauti muda mfupi.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Lutengano Mwakyoma, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kisha kutoa taarifa Kituo cha Polisi cha wilaya hiyo,ambapo walifika na kuthibitisha tukio hilo.

Hilo ni tukio la pili kutokea kwa wanafunzi wa shule mwaka huu,ambapo mwanzoni mwa mwaka mwanafunzi mwingine alifariki dunia baada ya kugundua kuwa ana ujauzito.
  
Aidha,mnamo majira ya saa 10 jioni Agosti 20 mwaka huu,katika Kijiji cha Ihanda,Wilayani Mbozi barabara ya Mbeya/Tunduma gari nambari T 466 BGF aina ya Toyota Coaster linalosafirisha abiria kutoka Mbeya mpaka Tunduma lilimgonga mtembea kwa miguu Moto Asha Mzumbwe(8) na kusababisha kifo papo hapo.

Hata hivyo chanzo cha ajali ya gari hilo lililokuwa likiendeshwa na dereva Bwana Michael Kasebele(56),mkazi wa Kalobe Jijini Mbeya,kimetajwa kuwa ni kuwa ni mwendokasi wa kupindukia.

Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na ametoa wito kwa wazazi kuchukua tahadhari ya kutowaacha watoto wao kurandaranda barabarani.

Tukio hilo nila kwanza tokea kuwekwa kwa matuta katika eneo la Ihanda,baada ya magari mengi kusababisha vifo vya mara kwa mara kwa wananchi wa eneo hilo,ambapo walifikia hatua ya kulichoma  moto gari ya abiria aina ya Coaster kutokana na mwendokasi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger