Pages


Home » » MATUKIO YA MKUTANO WA HADHARA ULIOJADILI MAUAJI YANAYOHUSISHWA NA IMANI ZA KISHIRIKINA - MBEYA

MATUKIO YA MKUTANO WA HADHARA ULIOJADILI MAUAJI YANAYOHUSISHWA NA IMANI ZA KISHIRIKINA - MBEYA

Kamanga na Matukio | 03:22 | 0 comments
Diwani wa Kata ya Myunga,Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya mheshimiwa Godfrey Siame kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)(kushoto),alipokuwa akimuonesha mpiga picha wetu moja ya kati ya makaburi saba yanayodaiwa kuwa waliozikwa waliuawa kwa imani za kishirikiana kisha kutolewa viungo vyao kama vile meno,sehemu za siri na Moyo pembezoni mwa Mto Momba.Hata hivyo zaidi ya watu watatu wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo hivyo hawajakamatwa licha ya kufahamika.
Wananchi wa Kijiji cha Myunga,Kata ya Myunga Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya wakisikiliza kwa makini mkutano wa hadhara uliokuwa unajadili mauaji ya kutisha yanayohusishwa na imani za kishirikina,ambapo baadhi waliouawa walinyofolewa viungo vyao kama vile meno,sehemu za siri na moyo.
Mwenyekiti wa Kijij cha Myunga Bwana Satieli Sikanyika akielezea kero ya wa mauaji yanayohusishwa na imani za kishirikina.
 Diwani wa Kata ya Tunduma mheshimiwa Frank Mwakajoka(kushoto) akimkabidhi pesa zenye thamani zaidi ya shilingi 200,000 Diwani wa Kata ya Myunga mheshimiwa Godfrey Siame zilizochangwa na wananchi katika mkutano kwa ajili ya kusaidia familia za watu 13 waliokamatwa katika Kata ya Myunga Agosti 11 mwaka huu wakituhumiwa kuharibu mali za mfanyabiashara Bwana Benard Simundwe ambaye pia anatuhumiwa kujihusisha na mauaji katika Kijiji cha Myunga.
Diwani Mwakajoka(kushoto) na Diwani Siame(kulia) wakihesabu fedha zilizochangwa na wananchi katika harambee iliyofanyika papo hapo katika mkutano.
 Mzee Sadock Simwanza ambaye alishindwa kujizuia kutoa machozi kutokana na matukio ya mauaji yanayofanyika katika kijiji cha Myunga.
Wananchi wenye hasira kali walishindwa kujizuia na kuamua kulipiza kisasi,kutokana na mauaji yaliyokithiri na Polisi kutochukua hatua zozote licha ya kuwasilishwa kwa vielelezo zikiwemo silaha mbili,simu za mkononi,nguo za baadhi ya marehemu ambazo Polisi walizichukua na kuwaachia huru watuhumiwa,ambapo baadhi ya Majambazi wawili waliuawa na wananchi,ambao walitumwa kwa ajili ya kumuua Diwani wa Kata ya Myunga Siame.
 (Picha na Ezekiel Kamanga, Myunga,Momba).
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger