Pages


Home » » MWENYEKITI WA KIJIJI AJIUZURU.

MWENYEKITI WA KIJIJI AJIUZURU.

Kamanga na Matukio | 04:49 | 0 comments
*Ni baada ya tuhuma za ubadhilifu wa shilingi 180,000/=H
*Akiri kuzilipa mkutanoni pesa anazodaiwa.
*Mjumbe wa Halmashauri ajimegea shilingi 424,400/=

Habari kamili na Ezekiel Kamanga,Mbarali.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Azimio Mswisi,Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya Bwana Luka Mwanyangwa amelazimika kujiuzuru pamoja na Halmashauri ya kijiji hicho baada ya kukiri kufuja pesa za kijiji hicho jumla ya shilingi 180000,zilizokuwa zimetolewa na mradi wa TASAF kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya kijiji hicho.

Mjumbe wa Halmashauri hiyo Bwana Daud Ngwale,anahusishwa kufanya ubadhilifu wa shilingi 424,400 ambapo inadaiwa kuzichukua fedha hizo katika akaunti ya kijiji na kuamua kuzitafuna badala ya kuzielekezea katika mradi uliokusudiwa.

Aidha,katika mkutano uliofanyika kijijini hapo Agosti 4 mwaka huu ulipobainika ufujaji huo na uliazimia viongozi hao kurejshewa pesa hizo mara moja vinginevyo wangefungwa kamba na kupelekwa Polisi ambapo Mwenyekiti Bwana Mwanyangwa alizilipa papo hapo shilingi 180,000 na kutangaza kujiuzuru uongozi huku mwenzake Bwana Ngwale akipewa muda hadi 1gosti 9 mwaka huu awe amezirejesha pesa hizo.

Hata hivyo Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bwana Tito Gerald Joha,amekiri kupokea pesa kutoka kwa mwenyekiti huyo wa kijiji na kujiuzuru kwake anatarajia kutoa muhtasari wa mkutano huo na kuwasilisha kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali kwa maamuzi zaidi.

Wakati huo huo,mbali na ubadhilifu huo,halmashauri hiyo imetumia zaidi ya shilingi 200,000 kwa ajili ya kuendesha kesi ya Bwna Robert Mwaigwisa,ambapo rai imetolewa kwa wote waliofanikiwa kwa wananchi kutojichukulia hatua  ya kisheria.

Habari ambazo zilikuwa zikiendelea nje ya mkutano huo zinadai kuwa mwenyekiti alishinikizwa kujiuzuru licha ya Bwana Mwanyangwa,kueleza ya kuwa yeye bado ni mwenyekiti halali wa kijiji hicho.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger