Pages


Home » » VUGU VUGU LA UCHAGUZI NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

VUGU VUGU LA UCHAGUZI NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

Kamanga na Matukio | 05:50 | 0 comments
 Na Esther Macha,Mbeya
Wakati vugu vugu la uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)likiendelea kushika kasi Rais wa Chama wakandarasi Wenyeji Tanzania(TLCO)Bw.Kura Mayuma amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Uenyekiti wa Mkoa wa Chama hicho Mkoani Mbeya.

Alisema kuwa lengo ni kushawishi  serikali kukataa  sheria na kanuni kandamizi kwa wananchi ambazo zimetungwa na Bunge n a mabaraza ya madiwani Mkoani hapa.

Bw. Mayuma alisema hayo  jana wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu za kugombea nafasi hiyo  katika Ofisi za chama cha mapinduzi zilizopo eneo la Sokomatola.

Alisema kuwa lengo la kugombea nafasi hiyo ni kutaka kurudisha hadhi ya chama hicho  Mkoani hapa ambacho tayari kimeppoteza mvuto kwa wanachama wake ili mwaka 2014 wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa uwe rahisi kupata viongozi wenye sifa.

“Pia katika uchaguzi huu kutawezesha kupata viongozi wenye sifa  kwa uchaguzi wa mwaka 2015 kwani tayari tutakuwa tumepata viongozi wenye sifa  ya kuongoza na hapa nimewingia kwa makusudi ili kuweza kukinusuru chama cha mapinduzi “alisema.

Alisema watu wanachaguliwa  katika chama watekeleze matakwa ya wananchi  badala yake wanashindwa kufanya yale waliyoagizwa  na hivyo kuanza kutokea vurugu  za wamachanga ambayo chanzo chake ni watendaji wa chini na hivyo CCM kuonekana kushindwa kuwajibika kwa wananchi.

Bw. Mayuma alisema hiyo inatokana na watendaji wa serikali kushindwa kuwajibika ,sera ya chama cha mapinduzi ni nzuri ila watendaji wake ndo wamekuwa tatizo kubwa.

Kwa Upande wake Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoani mbeya Bw. Maganga Sengelema alisema kwa sasa chama hicho kinajipanga vizuri ili kuweza kupata viongozi ambao watakitetea chama  tawala katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka 2014.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger