Pages


Home » » KWANINI WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE HAWAJIKITI KATIKA UANDISHI WA HABARI WA JINSIA YAO?

KWANINI WAANDISHI WA HABARI WANAWAKE HAWAJIKITI KATIKA UANDISHI WA HABARI WA JINSIA YAO?

Kamanga na Matukio | 05:45 | 0 comments
Habari na Ester Macha,Mbeya.
Kutokana na waandishi wa habari wanawake nchini kutojikita zaidi katika uandishi wa habari za wanawake imeelezwa kuwa hali hiyo  imesababisha  habari zinazohusu wanawake kutoripotiwa kwa undani zaidi na badala yake waandishi wa habari wanaume ndio wamekuwa wakiandika habari hizo.

Waandishi wa habari wanawake ndo wanatakiwa kuwa nguzo muhimu katika kuandika habari za afya hususani wanawake waliopo vijijini,wengi wanafahamu matatizo ya wanawake hivyo itakuwa rahisi kuripoti habari hizo kwa upana .

Mwito huo umetolewa  jana na Mkufunzi wa wa mafunzo ya habari za afya Dkt.Ahmed Twaha  wakati akitoa mada kwa waandishi wa habari wanaohudhulia mafunzo hayo ya siku nne ambayo yanaendeshwa na umoja wa  clabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC).

“Nyinyi kama waandishi wa habari wanawake  mnatakiwa kuwa wa kwanza  kuandika habari za afya kutokana na kuwa na uelewa zaidi kuhusu masuala ya wanawake kwa maradhi mbali mbali ambayo wanaugua,kwa uelewa wenu mtaweza kuandika kitu ambacho ni kizuri”alisema.

Alisema mara nyingi waandishi wa habari wanaume ndio wamekuwa wakiandika zaidi habari za afya tofauti na wanawake wenyewe ambao wana uelewa zaidi ,kuna umuhimu wanawake kuanza rasmi kujikita zaidi na uandishi wa habari hizi za afya.

Aidha Dkt.Twaha alisema kuwa wakati wa kuandika habari za afya ni muhimu kuandika  kwa takwimu sahihi  ili jamii iweze kupata taarifa ambayo imefanyiwa utafiti wa kina na kuelewa nini kinazungumzwa.

Hata Mkufunzi huyo alisema pia kuna umuhimu kuangalia changamoto zinazowakabili  wanawake waliopo vijijini kuhusiana na huduma za afya,na kwamba asilimia kubwa ya wanawake na watoto ndio wanaotibiwa katika hospitali kuliko wanaume.

Kwa upande wao waandishi habari wanawake wanaohudhulia mafunzo ya habari za afya walisema kuwa wanashindwa kuandika habari hizo  kutokana na kutokuwa na vitendea kazi pamoja na uwezeshaji wa kifedha kutokana na habari nyingi kuwa vijijini .

Mafunzo hayo yanaendeshwa na umoja wa clabu za waandishi wa habari Tanzania (UTPC)na yanajumuisha waandishi 18 kutoka Mkoa wa Mbeya.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger