Pages


Home » » MATUMIZI YA ARV MKOANI MBEYA YAMEKUWA YA HALI YA JUU.

MATUMIZI YA ARV MKOANI MBEYA YAMEKUWA YA HALI YA JUU.

Kamanga na Matukio | 03:32 | 0 comments
Na Bosco Nyambege ,Mbeya.
Mwitikio wa watu katika matumizi ya huduma ya ARV Mkoani Mbeya umebainika kuwa ni mkubwa.

Hayo ni kwamujibu wa kaimu mratibu wa kitengo cha UKIMWI mkoa wa Mbeya Dkt.Francis Philly alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jumatano hii.

Philly  amesema kuwa mwitikio wa wagonjwa wanaotumia dawa za ARV kuwa ni mkubwa kwani takwimu zinaonesha kuwa kuanzia June 2004 hadi June 2012 wagonjwa waliojiandikisha katika huduma ni 106598 ambapo watu wazima ni 92085 na watoto ni 12889.

Ameongeza kuwa kati ya hao walioanzishiwa dozi ya ARV ni 52903 ambapo watu wazima ni 40701 na watoto ni 12202 na watu 13163 hawajulikani kama wamekatisha dozi ama wameacha na katika hospitali ya mkoa wa mbeya watu 7675 wameandikashwa na 3539 wameanzishiwa tiba ya ARV na watu 1766 hawajulikani walipo na hali hii inaonesha wazi kuwa watu hawafuati maelekezo ya wataalamu wa afya .

Kwa takwimu hiyo inaonyesha kuwa zaidi ya 50%ya watu wote ambao wameandikishwa katika huduma CTC wameanzishiwa dawa.

Kwa upande wake Afisa muuguzi wa kitengo cha CTC katika Hospitali ya mkoa wa Mbeya Mariam Mhanjo amesema kuwa katika sekta hiyo wanakabiliwa na changamoto mbalimbali kama vile ukosefu wa vitendea kazi, upungufu wa wahudumu katika sekta hiyo,miundombinu mibovu hususani vijijini  pamoja na masilahi kuwa duni.

Hivyo Mhanjo ameiomba serikali kuweza kuwasaidia kutatua changamoto hizo   ili kuweza kufanya kazi katika mazingira mazuri na yanayorizisha.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger