Pages


Home » » UPUNGU WA VIFAA VYA MAABARA KATIKA HOSPITALI YA MKOA WA MBEYA.

UPUNGU WA VIFAA VYA MAABARA KATIKA HOSPITALI YA MKOA WA MBEYA.

Kamanga na Matukio | 05:49 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Upungufu wa  vifaa katika  kitengo cha Maabara katika hospitali ya Mkoa wa Mbeya umetajwa kuwa changamoto kubwa  ambayo inapelekea wagonjwa kuwa katika wakati mgumu  wa kupata vipimo muhimu .

Hayo yalisemwa jana na Mratibu wa Huduma za Maabara  katika hspitali ya Mkoa wa Mbeya Dkt.Ezekiel Tuya  wakati alipozungumza  na gazeti hili kuhusu matatizo ambayo yanakwamisha shughuli za maabara hosptalini hapo.

Alisema ukusefu huo wa vifaa unasababisha kuendelea kudorola kwa huduma , na tatizp kubwa  lingine ni upungufu wa wataalamu katika taaluma ya afya  hasa vitengo vya maabara  katika hospitali hiyo ambapo hali hiyo inasababisha  wanafdunzi kuyakimbia masomo ya sayansi  ambayo ndiyo msingi wa afya.

“Hili ni tatizop kwani mara nyingi wanafunzi wanaotaka kuja kufanya mazoezi wanashindwa kutokana na kutokuwa na kutokuwa na wataalamu wa hivyo ni jambo ambalo ni muhimu ambali serikali inatakiwa kulifanyia kazi , na hata huu ukosefu wa vifaa nao unatutesa sana hasa ukizingatia kipindi hiki ambacho tuna wagonjwa wengi ambao wanahitaji vipimo ili waweze kuazishiwa matibabu ya dawa”alisema.

Alisema tatizo linguine  ukosefu wa vifaa wa vifaa na vitendanishi  katika maabara vifaa ambavyo hurahisisha utendaji wa kazi  kwa watumishi wa maabara.

Hata hivyo Dkt. Tuya ameiomba serikali  kushughulikia ukosefu wa  wataalamu wa maabara nchini  ili kunusuru maisha ya watanzania wanafariki dunia kwa kukosa huduma ya vipimo kwa wakati .
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger