Pages


Home » » MTU MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA NYUMBA ALIYOKUWA AKIISHI KUCHOMWA MOTO NA WATU WASIOJULIKANA MKOANI MBEYA.

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA NYUMBA ALIYOKUWA AKIISHI KUCHOMWA MOTO NA WATU WASIOJULIKANA MKOANI MBEYA.

Kamanga na Matukio | 02:54 | 0 comments
 Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi.
*****
Na mwandishi wetu
 Mkazi mmoja wa Mbambo wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya Lastoni Mwangosi anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 40 hadi 50 amefariki dunia baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kuchomwa moto na watu wasiofahamika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amesema Bwana Mwangosi amefikwa na mauti jana majira ya saa 1 usiku baada ya nyumba yake kuchomwa moto.

Hata hivyo Kamanda Nyombi amemaliza kwa kusema  chanzo cha mauaji hayo ni imani za kishirikina na Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini aliyehusika na tukio hilo .
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger