Pages


Home » » BI ROSE MUHANDO AVURUGA MKUTANO WA INJILI KWA KUTOKUFIKA, LICHA YA KULIPWA MILIONI 2.5 MKOANI MBEYA

BI ROSE MUHANDO AVURUGA MKUTANO WA INJILI KWA KUTOKUFIKA, LICHA YA KULIPWA MILIONI 2.5 MKOANI MBEYA

Kamanga na Matukio | 05:05 | 0 comments
Baada ya kupewa mwaliko wa kutoa huduma ya neno la Mungu katika mkutano wa Injili  mkoani Mbeya na kushindwa kufika kwa Mwimbaji wa nyimbo za Injili Bi Rose Muhando, Pichani juu ni Bwana Riziki Mwakapugi akionesha stakabadhi za malipo ya benki(Pay in slip) ya shilingi milioni mbili nalaki tano zilizotumwa kwenye akaunti ya Mwimbaji huyo, kupitia benki ya Barclays. Mkutano huo wa injili ulioanza Novemba 18 hadi 20, mwaka huu  uliandaliwa na kanisa la Bethel Miracle Centre(BMC), Kituo cha Mbinguni lililopo eneo la Soweto jijini Mbeya.
 Jengo la Kanisa la Bethel Miracle Centre(BMC), Kituo cha Mbinguni lililopo eneo la Soweto jijini Mbeya, ambalo lilitoa mwaliko kwa Mwimbaji wa nyimbo za Injili nchini Bi. Rose Muhando, na kushindwa kufika licha ya kulipwa fedha taslimu shilingi milioni Mbili na nusu alizokuwa akizihitaji ili aweze kuhudhuria.
 Moja ya mabango yaliyotapakaa jiji zima likionesha muda, siku na mahali Mkutano wa injili utakapofanyika pamoja na wasanii wa nyimbo za Injili watakaotoa huduma ya neno la Mungu kupitia uimbaji, akiwemo Bi Rose Muhando, ambaye hakuweza kufika licha ya kuingiziwa kwenye akaunti yake shilingi milioni mbili na nusu alizokuwa akizihitaji ili aweze kuhudhuria.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger