Pages


Home » » WATUHUMIWA WATATU WA KUMILIKI NOTI BANDIA ZENYE THAMANI YA SHILINGI MIL 559,000/= WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA MARA YA PILI KATIKA MAHAKAMA YA MKOA WA MBEYA

WATUHUMIWA WATATU WA KUMILIKI NOTI BANDIA ZENYE THAMANI YA SHILINGI MIL 559,000/= WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA MARA YA PILI KATIKA MAHAKAMA YA MKOA WA MBEYA

Kamanga na Matukio | 06:05 | 0 comments
Na mwandishi wetu
Watu wa tatu wakazi wa Uyole jijini Mbeya wamepandishwa kizimbani kwa mara ya pili jana katika mahakama ya mkoa wa Mbeya, kusomewa shtaka la kumiliki noti bandia zenye thamani ya shilingi milioni tano, laki tano na elfu hamsini na tisa.

Akisoma kesi hiyo mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya Mkoa Mbeya mheshimiwa Fransis Kisheny na  mwanasheria wa serikali Grifin Mwakapeje amesema mnamo Novemba 17, mwaka huu  Emmanuel Mwandugule na Faraja Mwakibanza walikutwa na noti bandia zenye thamani ya  shilingi milioni tano na elfu tisa zilizo na namba mbili Noti zenye namba 142 BN 49393 na 268 BN 7949398.

Hata hivyo inadaiwa watuhumiwa hao walikimbia baada ya kuachiwa kwa dhamana katika kesi iliyosomwa Novemba 16, mwaka huu na hivyo kukamatwa tena.

Watuumiwa hao wamekana kosa la kutoroka, hali ambayo imemlazimu hakimu Fransis Kisheny kihairisha kesi hiyo hadi Novemba 30 mwaka huu na hivyo watuhumiwa kupelekwa rumande kwa kuhofia kutoroka tena.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger