Pages


Home » » TAMAA:- ADUNDWA MAKABURINI BAADA YA KUTAFUNA PESA ZA JENEZA

TAMAA:- ADUNDWA MAKABURINI BAADA YA KUTAFUNA PESA ZA JENEZA

Kamanga na Matukio | 05:11 | 0 comments
**Marehemu azikwa bila jeneza.
**Fundi aliyepewa pesa atorokea Mbeya.
**Watumishi wa Mungu washuhudia kichapo.
Habari na Ezekiel Kamanga.,
Bwana Marco Sikalunga Mkazi wa Kijiji cha Chilangawana,Sumbawanga Vijijini mpakani na Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya amenusurika kufikwa na mauti paacha ya kupokea kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali,baada ya kupewa jukumu la kuchangisha fedha shilingi 50,000 kwa ajili ya kuchonga jeneza.

Bwana Sikalunga alidai kuwa fedha hizo zilizochangishwa alimkabidhi fundi anayefahamika kwa jina la Senga na kwamba utakapofika muda wa saa za kuzika ataleta jeneza hilo.

Lakini katika mshangao mnamo Septemba 13 mwaka huu ulitokea msiba kijijini hapo,ambapo alifariki Suzana Upepo,na kijana huyo alipotakiwa kupeleka jeneza alidai anaenda kuchukua kwa fundi na alipofika nyumbani kwa fundi huyo hakufanikiwa kumkuta.

Kufuatia sakata hilo wananchi waliamua kuuchukua mwili wa marehemu na kwenda kuuzika bila jeneza,wakiwa njiani wananchi hao wakiwa na hasira kali walimpiga Bwana Sikalunga mbele ya Mchungaji Ladislaus Kamanga na Gidion .A. Simponda(Mwandete).
Hata hivyo Bwana Senga ambaye ni fundi aliyepewa jukumu la kutengeneza jeneza hilo anadaiwa kutorokea Mkoani Mbeya na kiasi hicho cha fedha cha shilingi 50,000.
Wakati huo huo wananchi hao wanatarajia kumchukulia hatua za kisheria Bwana Sikalunga.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger