Pages


Home » » MWANAFUNZI AANGUKA NA MTI NA KUPOTEZA MAISHA.

MWANAFUNZI AANGUKA NA MTI NA KUPOTEZA MAISHA.

Kamanga na Matukio | 05:27 | 0 comments
*Kichwa chake chapasuka na utumbo watoka nje.

 Habari na Ezekiel Kamanga,Sumbawanga Vijijini.
Mwanafunzi wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kilangawana,Kijiji cha Maleza,Kata ya Kapeta,Wilaya ya Sumbawanga Vijijini Mkoani Rukwa aitwaye Imani Nzala(12),amefariki dunia baada ya kudondokewa na mti ulikokuwa ukikatwa na Babu yake Bwana Nzala kwa ajili ya kuchomea tanuli la tofali.

Katika ajali hiyo ya kusikitisha iliyotokea Septemba 16 mwaka huu majira ya saa tano,mtoto huyo alipasuka kichwa na utumbo wake kutoka nje hali iliyopelekea kukimbizwa hadi Kituo cha Afya cha Kilangawana.

Licha ya marehemu kukimbizwa katika kituo hicho akiwa bado hajafariki,Muuguzi wa kituo hicho aliomba Imani awaishwe hadi Kituo cha Afya cha Kamsamba,ambako huko kutokana na tatizo hilo kuwa kubwa waliomba asafirishwe hadi Hospitali ya Wilaya ya Mbozi,lakini kabla ya gari la wagonjwa kufika mwanafunzi huyo alifarikia dunia.

Hata hivyo Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Kamsamba Bwana Michael Kajemi,amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba kifo cha mwanafunzi huyo kimetokana na kuvuja damu nyingi katika mwili wake.

Mazishi ya kuupumzisha mwili wa marehemu Imani,kwenye nyumba yake ya milele yamefanyika Septemba 17 mwaka huu kijijini kwao.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger