Pages


Home » » NOTI ZA SHILINGI 500 NA 2000 ZA HARIBIWA KWA AJILI YA KUTENGENEZA POMBE AU KUVUTIA SIGARA.

NOTI ZA SHILINGI 500 NA 2000 ZA HARIBIWA KWA AJILI YA KUTENGENEZA POMBE AU KUVUTIA SIGARA.

Kamanga na Matukio | 05:26 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Sumbawanga Vijijini.
Taifa linaweza kuingia katika hatari ya kudidimia kwa uchumi kufuatia watu wasiokuwa na mapenzi na taifa hili kuziharibu noti za shilingi 500 na 2000 kwa kuondoa mstari(ufito) unaong'aa na unaohalalisha pesa hizo na kisha kuutumia katika pombe za kienyeji au bia ili kuongeza kileo wakidai kuwa husaidia kuokoa pesa kwani hulewa kwa muda mfupi.

Mbali na hivyo mstari huo(ufito) pia huzichanganya na sigara au tumbaku ambapo hudai hulewa haraka,hivyo kufanya uadimu wa noti hizo katika maeneo ya Kijiji cha Maleza,Kata ya Kipeta,Wilaya ya Sumbawanga Vijijini.

Athari hiyo pia imevikumba vijiji vya Kilangawana na Kamsamba hali ambayo imefanya kuwepo kwa ugumu wa upatikanaji wa fedha hizo.

Hata hivyo wananchi kadhaa ambao hawakupenda majina yao kutajwa,wamethibitisha kutokea kwa matukio hayo na kuitaka Serikali na Benki Kuu kuchukua hatua za haraka ili kukomesha vitendo hivyo.

Katika hali ya kuhalalisha noti hizo zilizoharibiwa wahalifu hao hutumia gundi kwa kutumia uzi wa mifuko ya mbolea ili ziendelee kutumika na hivyo kuzalisha noti bandia.

Wakati huohuo wananchi wanatakiwa kuchukua tahadhari mapema wanapopokea noti hizo na pia kuwafichua wahalifu hao.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger