Pages


Home » » KUSHUKA KWA UWAJIBIKAJI NA UTENDAJI KAZI WA WATUMISHI WA IDARA MBALIMBALI

KUSHUKA KWA UWAJIBIKAJI NA UTENDAJI KAZI WA WATUMISHI WA IDARA MBALIMBALI

Kamanga na Matukio | 05:32 | 0 comments
Na Gabriel Mbwille, Mbeya.
Imedaiwa kushuka kwa uwajibikaji na utendaji kazi wa watumishi wa idara mbalimbali hapa nchini vikiwemo vyombo vya habari kukosa maadili kunatokana na mfumo mbovu wa elimu ya hapa nchini.

Hayo yalisemwa na waandishi wa habari mkoani Mbeya wakati wa mafunzo ya uandishi wa habari kwa njia za mtandao ambayo yameandaliwa na umoja wa klabu za wa andishi wa nchini  (UTPC) yaliyofanyika katika ukumbi wa hospitali ya mkoa Mbeya.

Walisema kuwa hivi sasa kumekuwa na tabia ya ajira kutolewa kwa kuangalia kigezo cha elimu pekee pasipo kuangalia ujuzi na uzoefu wa mfanyakazi kikazi na kimazingira haliinayopelekea kuajiliwa kwa watu waio na ufahamu wowote wa kile wanachokifanyia kazi.

Mmoja wa washiriki wa mafunzo Saidi Benjamini alisema hivi sasa ni jambo la kawaida kwa mtu kuajiliwa mara baada ya kumaliza mafunzo pasipo kupewa elimu ya mazingira ya kazi hali inayopelekea idadi kubwa ya watumishi wa Serikali kudanga takwimu kwa jamii na taifa.

Naye mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi Hawa Mathias alisema kutokana na teknolojia kukua baadhi ya watumishi wamekuwa wakitumia takwimu na tafiti kutoa elimu kwa wananchi pasipo kuangalia uhalisia wa eneo husika na kwamba tabia hiyo imekuwa ikichangia kwa sehemu kubwa elimu inayotolewa ndani ya jamii kutofanikiwa kwa sehemu kubwa kutokana na kutoendana na uhalisia wa eneo husika.

Naye mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari mkoani Mbeya Christopher Nyenyembe alisema kuwa utafiti kabla ya kuandika habari ni moja ya taratibu za kazi kwa mwandishi bora na kuwataka waandishi wa habari kufanya tafiti kwakina ndani ya jamii kabla ya kuiandika habari badala ya kutumia tafiti zilizopo kwenye mitandao kwa sababu tafiti nyingine zimekuwa haziendani na uhalisia wa mazingira ya kazi.
 
Kwa upande wake mkufunzi wa mafunzo hayo Maggid Mjengwa alisema tabia ya Serikali kuangalia zaidi vyeti vya elimu ndiyo matokea ya sasa kwa wanafunzi kuhitimu elimu yao ya msingi pasipo kujua kusoma wala kuandika.

Aidha tabia ya kuaingiza siasa na maarifa imekuwa ikichangia kwa sehemu kubwa kukwamisha maendeleo ya elimu hapa nchini ambapo hivi karibuni tumeona Taifa limeamua kuacha mfumo wa mwanafunzi kuonesha nini amejifunza kwa kipindi chote na tumeingia kwenye mfumo wa mwanafunzi kukisia majibu.

"Hivi karibuni Tanzania imengia kwenye mfumo wa usahihishaji wa mitihani ya darasa la saba kwa njia ya mtandao ambapo wanafunzi watakuwa wakiweka vivuli kwenye majibu sahihi badala ya wanafunzi hao kuonesha uwezo walionao kutokana na yale waliyofundishwa ambapo hii inahatarisha zaidi kwa taifa kuwa na wanafunzi wasio na uelewa na elimu kwa sababu ya kuandika majibu yao kwa njia ya kukisia pia huenda ikawa ni njia kubwa ya wanafunzi kupewa majibu ya mtihani kuliko hata tatizo la awali lililojitokeza"alisema Mjengwa
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger