Pages


Home » » MWENYEKITI WA KIJIJI AKATA MITI YA SHULE BILA RIDHAA YA KAMATI

MWENYEKITI WA KIJIJI AKATA MITI YA SHULE BILA RIDHAA YA KAMATI

Kamanga na Matukio | 05:06 | 0 comments
*Kamati yacharuka yamtaka alipe fidia.
*Vijana watishia kikao cha ndani.
*Diwani akanusha kumbeba mwenyekiti.

Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Motomoto Bwana Kassimu Mwagala,amejikuta katika wakati mgumu baada ya kuitwa na Kamati ya Shule ya msingi Motomoto alipotakiwa kutolea maelezo suala la kukata miti saba ya shule hiyo kutokana na shinikizo la vijana kutaka kuongeza uwanja wa shule pasipo ridhaa ya kamati hiyo.

Akiongea kwa masikitiko Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Bi Lydia Mdoe,amesema kitendo hicho kilichofanywa na mwenyekiti huyo nicha dharau,hivyo kuwafanya waishi kwa hofu shuleni hapo licha ya dhamana waliyopewa na Serikali ya kulinda mali za shule na mazingira yetu.

Aidha Mwenyekiti wa Kamati ya shule hiyo Bwana Yusuph Tosha amesema ukataji wa miti hiyo uliofnya na Mwenyekiti wa kijiji ni kuifanya kamati yake kuonekana haifanyi kazi na ni kuingilia majukumu.

Hali hiyo ilizua taflani katika kikao ambapo Bwana Mwagala kwa kujihami aliandamana na kundi la vijana,ambao walifanya fujo katika mkutano na baadae Diwani wa Kata ya Ruiwa mheshimiwa Alex Mdimilage aliagiza kuwa vijana wote waitwe Ofisi ya kata watoe maelezo ni kwani walivamia mkutano usiowaruhusu.

Hata hivyo kutokana na kukera na kitendo cha Mwenyekiti wa kamati hiyo ilimtaka kulipa jumla ya shilingi 210,000 ili iwe onyo kwake,ambapo ametakiwa kuomba radhi,kamati hiyona kutakiwa kuzilipia kabla ya Oktoba 12 mwaha huu.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger