Pages


Home » » DIWANI ATISHIWA KUUAWA

DIWANI ATISHIWA KUUAWA

Kamanga na Matukio | 05:27 | 0 comments
Diwani wa Kata ya Myunga,Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya mheshimiwa Godfrey Siame kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)(kushoto),alipokuwa akimuonesha mpiga picha wetu moja ya kati ya makaburi saba yanayodaiwa kuwa waliozikwa waliuawa kwa imani za kishirikiana kisha kutolewa viungo vyao kama vile meno,sehemu za siri na Moyo pembezoni mwa Mto Momba.Hata hivyo zaidi ya watu watatu wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo hivyo hawajakamatwa licha ya kufahamika.
*******
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbozi.
Diwani wa Kata ya Myunga,Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya Mheshimiwa Godfrey Siame,amedai kutishiwa kuuawa na wafanyabiashara watatu waliopo Wilaya Momba na Mbozi mkoani hapa.

Hayo yamethibitishwa na diwani huyo baada ya awali Majambazi wawili waliokodiwa kutoka Mkoani Morogoro kuuawa na wananchi wenye hasira kali,ambapo kabla ya mauti majambazi hao walikiri kwa maandishi na kuibua siri nzito kuwa wao wametumwa na Mfanyabiashara Benard Simundwe, Kasambilo Mteka na Yohana Simkonda wote wakazi wa Kijiji cha Myunga.

Aidha Diwani Siame amesema kuwa wananchi walifanikiwa kukamata silaha mbili aina ya Short Gun ambazo zilikuwa maalumu kwa ajili ya mauaji yake,simu mbili zenye SMS ya kutumiwa pesa kutoka kwa wafanyabiashara hao.

Hata hivyo vielelezo vyote hivyo vilikabidhiwa kwa Mkuu wa Kituo cha Jeshi la Polisi Mji mdogo wa Tunduma mkoani hapa Bwana Wendo na taarifa kutolewa kwa Mkuu wa kituo cha Polisi wilaya ya Mbozi Bwana Dudu,lakini cha kushangaza zaidi mpaka sasa watuhumiwa hao hawajakamatwa na kufikishwa mahakamani licha ya kuwepo kwa vielelezo hivyo.

Imedaiwa kufuatia tuhuma mbalimbali dhidi ya wafanyabiashara hao ambao pia wamedaiwa kujihusisha na mauaji ya kikatili kijijini hapo,Jeshi la polisi linawashikilia wananchi 14,ambao wanadaiwa kuibomoa na kuiteketeza kwa moto nyumba ya Mfanyabiashara Simundwe.

Wananchi waliokamatwa na kufikishwa mahakama ya Wilaya Mbozi kusomewa shtaka la kesi ya jinai ya wizi wa kutumia silaha na kupora mali ni Alick Siame, Hosea Sinsungwe, Amani Siame, Musa Siame, Laurent Simsokwe, Lighton Sichone, Sadock Simwanza.

Wengine ni Osphat Siame, John Simbeye, Jacob Mwakalibule, Paulo Sichona na katika kesi hiyo watoto wawili waliopo chini ya miaka 18 wamehusishwa katika sakata hilo ambao ni Damas Sinzumwi na Zebius Sinzumwi.

Watuhumiwa wote wamenyimwa dhamana,ambapo kesi yao imeahirishwa na Hakimu Mushi na itatajwa tena Septemba 24 mwaka huu na watuhumiwa wote wanatetewa na Wakili wa kujitegemea mheshimiwa Edgar Bantulaki.

Kwa upande wake mwendeshwa mashtaka wa Serikali anatarajia kurekebisha mashtaka baada ya kupata marekebisho kutoka kwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Mbeya Diwani Athumani ambapo jalada limewasilishwa kwake.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida simu mbili zilizokuwa na vielelezo zimekabidhiwa kwa ndugu wa marehemu waliouawa kitu ambacho kimewashangaza watetezi wa haki za binadamu akiwemo Mwenyekiti wa mkoa wa Mbeya Bwana Said Mwadudu,hali inayotia shaka hali ya utendaji kazi wa Polisi kituo cha Tunduma na Mbozi kwa kushirikiana na wahalifu.

Diwani Siame alitoa taarifa za kutishiwa kwake kuuawa,lakini amedai kusikitishwa na kitendo cha Polisi kushindwa kuwakamata watuhumiwa na hata Septemba 10 mwaka huu mfanyabishara Benard Simundwe alionekana mahakamani na baadae kuamuliwa na mmoja wa askari wa polisi alimuondoa eneo la tukio na mfanyabishara biasharaa huyo kuelekea kituo cha polisi Mbozi hali iliyowashangaza wananchi kwa polisi kudai hapatikani.

Vituo vya Polisi vya Tunduma,Mlowo na Mbozi vimedaiwa kuwakumbatia wahalifu na hivi sasa diwani huyo amekuwa akilindwa na wananchi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger