Pages


Home » » SIKU AMBAYO SERIKALI YA KIJIJI CHA IYOVYO ILIYOTOONDOLEWA MADARAKANI.

SIKU AMBAYO SERIKALI YA KIJIJI CHA IYOVYO ILIYOTOONDOLEWA MADARAKANI.

Kamanga na Matukio | 02:55 | 0 comments

 Jinsi alivyokuwa akiondoka mkutanoni Mwenyekiti wa Kijiji cha Iyovyo,Kata ya Totowe,Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya Bwana Rashid Likuta mara baada ya kuvuliwa madarakani kwa kile kilichodaiwa kuwa anajihusisha na ufujaji wa pesa za kijiji wa zaidi ya shilingi laki nne na kutosoma taarifa za mapato na matumizi.
 Baadhi ya Wajumbe walioteuliwa kuchunguza ubadhilifu wa pesa za Kijiji cha Iyovyo,wakikamilisha taarifa kabla ya kuisoma.
 Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wakisikiliza kwa umakini mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Kijiji cha Iyovyo,Bwana Rashid Likuta.akijitetea kuhusiana na tuhuma zinazomkabili..
 Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wakisikiliza kwa umakini mkutano huo.
 Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Iyovyo Bwana Njobeni,aliyepewa madaraka ya kukaimu nafasi ya Uafisa Mtendaji wa kijiji mara baada ya Serikali ya kijiji kutenguliwa madarakani kutokana na ufujaji wa fedha za kijiji..
 Diwani wa Kata ya Totowe mheshimiwa Godian Wangala,akiwasihi wananchi kuendelea kuchangia maendeleo licha ya Halmashauri ya Kijiji kuondolewa madarakani kutokana na ubadhilifu wa fedha za kijiji.
 Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi Bwana Michael Mwamlima,akitoa taarifa za kubaini ubadhilifu huo uliofanywa na uongozi wa kijiji katika mkutano wa kijiji.
Meza na viti vikiwa wazi baada ya viongozi wa kijiji kuvuliwa madarakani(Picha na Ezekiel Kamanga,Mbeya).
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger