Pages


Home » » HAKIMU ALIYETUHUMIWA KWA RUSHWA AACHIWA HURU

HAKIMU ALIYETUHUMIWA KWA RUSHWA AACHIWA HURU

Kamanga na Matukio | 04:47 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Mbeya,umemwachia huru aliyekuwa Hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Mbeya Amani Mwihomeke(30),aliyekuwa anakabiliwa na tuhuma za rushwa.

Hakimu huyo anakabiliwa na makosa mawili kinyume cha sheria kifungu cha 15 cha kanuni ya adhabu kifungu kidogo(i) cha 11/2007 ambapo alidaiwa kushawishi na kupokea rushwa ya shilingi 150,000 mnamo Mei 29 mwaka huu.

Mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka kikosi cha kupambana na kuzuia rushwa nchini TAKUKURU,Kanda ya Mbeya Bwana Nimrod Mafwele akisaidiwa na Sarah Martin walidai Mahakamani kuwa Amani Mwihomeke alishawishi na kupokea rushwa hiyo katika Bar ya Bonanza iliyoko barabara ya Benki Kuu Jijini Mbeya.

Hakimu mfawidhi wa wilaya ya hiyo a Seif M. Kulita amesema mtuhumiwa anaachiwa huru kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha tuhuma hizo hivyo mahakama kuchukua uamuzi huo wa hukumu ambayo ilichukua masaa matatu kusomwa katika mahakama hiyo.

Hakimu Mwihomeke alikuwa anatetewa wakili wa kujitegemea Mika Thadayo Mbise.

Hata hivyo Hakimu mfawidhi Kulita alitaka waeshesha mashtaka kuandaa vema mashtaka ambapo wameshindwa kuthibitisha tuhuma ambazo zingemtia mtuhumiwa hat
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger