Pages


Home » » AFISA MTENDAJI WA KIJIJI MATATANI KWA KUFUJA PESA NA MIFUKO YA SARUJI.

AFISA MTENDAJI WA KIJIJI MATATANI KWA KUFUJA PESA NA MIFUKO YA SARUJI.

Kamanga na Matukio | 05:45 | 0 comments
Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
Afisa mtendaji wa Kijiji cha Idimi,Wilaya ya Mbeya Vijijini Mkoani Mbeya Bwana Amon Myola,ameingia matatani kwa tuhuma za kufuja pesa za michango shilingi 190,000 kati ya shilingi 746,000 pamoja na mifuko 16 kati ya 30 iliyotolewa na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Mchungaji Luckson Mwanjale.

Hayo yamebainishwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika Julai 12 mwaka huu kijijini hapo na kusimamiwa na Afisa Utumishi wa halmashauri ya wilaya hiyo Bwana Kernslave Wensle Mpoto.

Pesa hizo zilichangwa na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Idimi iliyoezuliwa Desemba 24 mwaka uliopita.

Aidha imedaiwa kuwa Bwana Myola,amekuwa akiendesha kamati ya ujenzi wa shule pekee yake hali iliyopelekea kuwepo kwa hasara na wananchi kugomea kuendelea kutoa michango ambapo matarajio ilitakuwa kukusanywa shilingi milioni 11.

Katika Mkutano huo aliagizwa na Afisa Utumishi Bwana Mpoto kuzirejesha fedha hizo na mifuko hiyo ya saruji katika mkutano wa hadhara ujao utakaofanyika Julai 20 mwaka huu.

Hata hivyo juhudi za kumuondoa madarakani Mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Yohana Bahati na halmashauri yake,zilishindikana baada ya tuhuma zilizowasilishwa katika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Mbeya kukosa nguvu za kumtia hatiani.

Agizo likatolewa kwa viongozi wa vitongoji kuhakikisha michango yote inayochangwa na wananchi imewasilishwa kwa Afisa Mtendaji wa Kata kabla ya tarehe hiyo iliyopangwa kwa ajili ya mkutano ujao wa hadhara.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger