Pages


Home » » Serikali imekubali mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la soka nchini TFF.

Serikali imekubali mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la soka nchini TFF.

Kamanga na Matukio | 01:53 | 0 comments
  Rais wa shirikisho la soka nchini TFF Leodger Chilla Tenga 
 =====
Na Shaban Kondo,
Serikali imekubali mchakato wa uchaguzi wa Shirikisho la soka nchini TFF uendelee kwa sharti la kuhakikisha haki inatendeka kwa wagombea waliofika mbele ya Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi iliyo chini ya mwanasheria Iddy Mtiginjola.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kikao kilichoketi jana kati ya uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo chini ya Waziri Dk. Fenella Mukangara, TFF pamoja na Baraza la Michezo la Taifa (BMT).

Amesema baada ya makubaliano hayo, TFF italiandikia barua Shirikisho la soka duniani FIFA ambalo lilisimamisha mchakato wa uchaguzi mwezi uliopita kwa ajili ya kutuma ujumbe ambao unatarajia kuja nchini kusikiliza malalamiko ya wagombea walioenguliwa.

Katika hatua nyingine raisi Tenga amewakumbusha wanachama wa TFF, hasa wajumbe wa Mkutano Mkuu kufahamu kuwa TFF ina katiba, lakini ni lazima pia wafahamu kwanini kuna FIFA.

Rais Tenga amewakumbusha wanachama wa TFF ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu wanaopita mikoani kuomba saini za wajumbe ili kuita Mkutano Mkuu wa dharura wakati wanajua mkutano ulishaitishwa, lakini ukasimamishwa na FIFA.

Wakati huo huo mwenyekiti wa baraza la michezo la taifa BMT Dioninz Malinzi ambae aliuwakilisha upande wa serikali katika mkutano na waandishi wa habari amesema hawana shaka na maafikiano yaliyofikiwa baina yao, lakini kikubwa akasisitiza taratibu walizoagiza zinastahili kufuatwa za kuwatendea haki walioenguliwa kwenye mchakato wa uchaguzi.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger