Pages


Home » » Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya linawashikilia wahamiaji haramu wanne raia wa Ethiopia .

Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya linawashikilia wahamiaji haramu wanne raia wa Ethiopia .

Kamanga na Matukio | 05:22 | 0 comments


Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.

Jeshi la polisi mkoa wa Mbeya linawashikilia wahamiaji haramu wanne raia wa Ethiopia kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.



Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Barakiel Masaki amesema watu hao wamekamatwa kutokana na ushirikiano mzuri uliopo kati ya polisi na madereva Tax wa maeneo ya Uyole.



Amewataja waliokamatwa kuwa ni  Tarafa Mgomewa mwenye umri wa miaka 18, Mlegeta Tadesa mwenye umri wa miaka 18, Damaka Lama mwenye umri wa miaka 20 na Nighato Tagenya, mwenye umri wa miaka 22 wote raia wa Ethiopia.



Aidha watuhumiwa wote wanatarajiwa kufikishwa idara ya uhamiaji kwa hatua zaidi za kisheria na kutoa wito kwa jamii kuendelea kutoa ushirikiano na jeshi la polisi ili kudhibiti vitendo vya uhalifu mkoani hapa.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger