Pages


Home » » Aoa Mwanafunzi wa kidato cha pili kwa Ng’ombe 45.

Aoa Mwanafunzi wa kidato cha pili kwa Ng’ombe 45.

Kamanga na Matukio | 02:21 | 0 comments
·       Aoa Mwanafunzi wa  kidato cha pili kwa Ng’ombe 45.
·       Atishia kuua wanaomfuatilia.
·       Mwanafunzi arudishwa kwa wazazi wake kukwepa mkono wa Sheria.
Na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Mtu mmoja mkazi wa Kijiji cha Mpona Kata ya Totowe Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya anatuhumiwa kumwachisha masomo mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Totowe    kwa kumuoa  kisha kumpa ujauzito.
 
Mwananchi huyo aliyefahamika kwa jina la Shigala Mwachanya anatuhumiwa kutenda kosa hilo kwa kumpa ujauzito mwanafunzi aliyejulikana kwa jina la Ngolo Jiguma(19) ambaye amesitisha masomo yake kutokana na ujauzito alionayo ambapowazai walipatana kulipana Ng’ombe 45 kama fidia ambapo tayari Ng’ombe 20 wameshatolewa.
 
Aidha kutokana na Mwanafunzi huyo kutambua kuwa  Wazazi wake wametenda kosa ameamlia kuto hudhulia kliniki katika kituo cha afya cha Malangali na badala yake amekuwa akienda katika Zahanati ya Totowe ili kukwepa kukutwa na vyombo vya sheria.
 
Uongozi wa  Kijiji hicho umeanza kulifuatilia sakata hilo baada ya kupata taarifa kutoka kwa Mkuu wa Shule aliyokuwa akisomaMwanafunzi huyo Frank Mwakisyala ambapo juhudi hizo zinaonekana kugonga ukuta kutokana na kutishiwa kuawa na mtuhumiwa.
 
Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho Yaledi Mwanguku aliwaambia waandishi wa Habari kuwa suala hilo lipo juu ya uwezo wake hivyo alilazimika kulipeleka suala hilo kwenye uongozi wa kata kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.
 
Diwani wa Viti Maalumu kata hiyoChristina Kibwana ambaye alionekana kulipokea suala hilo na kuanza kulifuatilia pia alidai kuwa alipokea ujumbe mfupi wa maandishi ukimtaka ahame kijijini hapo lasivyo aache kulifuatilia sakata hilo na asipoachaangeuawa.
 
Diwani huyo alisema ujumbe huo wenye maneno ya kutishia yalikutwa kwenye barua nje kidogo nje ya nyumba yake ambapo aliongeza kuwa baada ya kuona hali hiyo aliamua kutoa taarifa katika kituo  kidogo cha Polisi cha Galula Wilayani Chunya.
 
Diwani huyo aliendelea kulalamika kuwa baada ya kutoa taarifa katika kituo hicho hakuna dalili wala hatua zozote zilizochukuliwa ambapo alisema kuna dalili za Rushwa ambayo inasemekana kuwa Polisi walipewa Rushwa ya Shilingi Milioni Moja na Nusu(1500,000/=).
 
Alisema kutokana na kutoonekana kwa hatua zozote aliamua kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Chunya ambapo walimkamata mtuhumiwa huyo kisha kufunguliwa kesi katika Mahakama ya Wilaya ya Chunya.
 
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Totowe kupitia Chama cha Mapinduzi, Godian Wangala  alithibitisha kutokea kwa matukio yote hayo na kuongeza kuwa amesikitishwa na kitendo cha Mwananchi huyo pamoja na wazazi kwa kumwachisha masomo na kumsababishia Mwanafunzi kumnyima haki ya kupata elimu.
 
Alisema Elimu ni haki ya msingi ambayo ingeweza kumkomboa kifikra na Serikali kufikia malengo yake ya kutoa elimu kwa wote kwa kuhimiza ujenzi wa shule za kata na kuongeza kuwa Mwanafunzi huyo amekuwa akiyumbishwa kutokana na kukatishwa mahudhurio ya Kliniki.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani  amekiri kupokea taarifa hizo na kuahidi kulifanyia kazi kwa ukaribu zaidi na kuhakikisha wahusika watachukuliwa hatua zinazostahili.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger