Pages


Home » » Halmashauri ya jiji la Mbeya imetoa zaidi ya shilingi milioni 18 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vyumba 24 vya madarasa'

Halmashauri ya jiji la Mbeya imetoa zaidi ya shilingi milioni 18 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vyumba 24 vya madarasa'

Kamanga na Matukio | 05:21 | 0 comments



Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.

Halmashauri ya jiji la Mbeya imetoa zaidi ya shilingi milioni 18 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vyumba 24 vya madarasa katika shule ya Sekondari Nzondahaki iliyopo kata ya Nzovwe.



Akiongea na Mwandishi wa habari hii Afisa mtendaji wa kata hiyo Furaha Malele amesema fedha hiyo itasaidia kukamilisha vyumba vya madarasa 24 kati ya vyumba 32 vilivyopo kwenye shule hiyo.



Amesema fedha hizo zitatumika katika kununua saruji kwa ajili ya sakafu na ripu, mbao za kenchi, mabati ikiwa ni pamoja na kugharamia kupaka chokaa kwenye vyumba vyote 24.



Wakati huohuo ameahidi kukamilisha ujenzi wa vyumba hivyo ndani ya siku 7 ili kuwawezesha wanafunzi kuendelea na masomo yao katika hali nzuri.
Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger