Pages


Home » » WANANCHI WA KATA YA MAGAMBA WILAYANI CHUNYA WAIKATAA TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI YA KATA YAO

WANANCHI WA KATA YA MAGAMBA WILAYANI CHUNYA WAIKATAA TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI YA KATA YAO

Kamanga na Matukio | 02:26 | 0 comments

Kapala  Chakupewa Makelele Diwani wa kata ya Magamba Chunya na pia ndiye mwenyekiti wa ccm na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya chunya ndiye taarifa yake ya mapato na matumizi imekataliwa na wananchi wake
Kaimu mtendaji wa kata ya Magamba Festo Pandisha akijaribu kuwafafanulia vizuri taarifa hiyo ya mapato na matumizi 
Wananchi wakiwa makini kuwasikiliza viongozi wao wakiwasomea mapato na matumizi ya kijiji chao
Mwenyekiti naona hapo unapindisha mahesbu kuwa mkweli kama pesa mmetafuna tupe jibu la uhakika
Waheshimiwa hapo mbele naona mnatuyumbisha leo tunataka kujua ukweli wa pesa zetu
Naombeni mkajipange upya hatukubali hayo mahesabu
Kila mwananchi alinyoosha kidole kwa meza kuuu kupinga taarifa hiyo
Huku kikao kikiendelea vinywaji moto na baridi viliendelea kuuzwa katika mkutano huo ambao umefanyika kilabuni 
Mambo yanaendelea kikaoni hapo hivi kweli kikao kufanyikia kirabuni ni sawa? maana hatuna uhakika kila litakaloongewa hapo likaungwa mkono maana wengi watakuwa tayari wamelewa

WANANCHI wa kata ya Magamba Wilaya ya Chunya Mkoani hapa wameikataa taarifa ya mapato na matumizi iliyosomwa na Diwani wa kata hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Wilaya na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.
  
Mwenyekiti huyo Kapala Chakupewa,alipatwa na mkasa huo hivi karibuni alipokuwa akiwasomea wananchi mapato na matumizi ya kata hiyo kutokana na utaratibu wa Serikali unaotaka wananchi kujua matumizi ya fedha walizochanga kwa ajili ya matumizi ya shughuli za maendeleo.
  
Taarifa iliyokataliwa na wananchi hiyo ilikuwa ni taarifa ya miezi sita(6) iliyokuwa inahusu mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha kata hiyo kutokana na mchango wa wakazi hao ulioanza kuchangishwa tangu mwaka 2007 na kufikia jumla ya Shilingi Milioni 7.
  
Sababu za wananchi hao kukataa taarifa hiyo ni kutokana na kile walichodai kuwa fedha hizo hazijafanya kazi yoyote ambapo Mwenyekiti huyo alisoma kama fedha hizo zimetumika hali iliyosababisha wananchi hao kuhoji eneo walilotumia fedha hizo ambapo baadaye Mwenyekiti huyo alibatilisha kauli yake kuwa hazijatumika.
  
Aidha wananchi hao wameendelea kuhoji kuwa ni kwa nini fedha za umma zitunzwe mikononi mwa watu binafsi badala ya kutunza katika taasisi za fedha pamoja na kutoanza kwa ujenzi huo kwa zaidi ya miaka Mitano tangu waanze kuchangishwa fedha hizo.
  
Hata hivyo kutokana na kutoridhika na mwenendo wa matumizi ya fedha hizo wananchi hao kwa ujumla wao waliamua kuwa ujenzi wa kituo cha afya usitishwe na fedha zilizochangwa zirejeshwe kwa kila kijiji kulingana na michango yao.
  
Akijibu tuhuma hizo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Magamba, Mwenyekiti huyo Kapala Chakupewa, amesema sababu za kutoanza kwa ujenzi huo kwa wakati   ni  kutokana na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kutotoa Gari la kusombea mawe kama walivyokuwa wameahidi awali.
  
Amesema baada ya kuomba gari kwa mkurugenzi aliambiwa gari hilo ni bovu hivyo halitaweza kufanya kazi ya kusomba mawe ndiyo maana ikamlazimu kuahirisha zoezi la ujenzi wa kituo cha afya hadi gari litakapopatikana lenye uwezo wa kufanya kazi.
  
Pia Mwenyekiti huyo amekiri kuwa Kaimu Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Festo Pandisha kuwa anadaiwa zaidi ya Shilingi Laki nne (400,000/=) ambazo alichangisha kutoka kwa wananchi kwa ajili ya ujenzi wa Shule lakini Mtendaji huyo alisema hajui zilipo licha ya kukiri kuzipokea kutoka kwa wananchi.
  
Aidha pia Mtendaji huyo aliahidi kuzirejesha fedha hizo kwa kununua saruji yenye thamani ya Shilingi laki nne kwa ajili ya ujenzi wa shule lakini hajafanya hivyo hadi siku taarifa ya fedha inasomwa hadi wananchi kuikataa.
  
Kutokana na kauli za Mwenyekiti huyo kuonekana kumtetea Mtendaji na kudidimiza maendeleo ya kata, Wananchi wameamua taarifa hiyo ikaandaliwe upya ili isomwe wiki ijayo na fedha zote zirudishwe kwa ajili ya matumizi mengine ambayo wananchi wenyewe wataamua.
  
Wamesema endapo fedha hizo na taarifa hazitaandaliwa upya na kwa usahihi basi watapeleka malalamiko yao kwenye ngazi za kisheria ili hatua zingine ziweze kuchukua  mkondo wake ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti na Mtendaji kuwajibishwa kwa ubadhilifu na uzembe.
  
Hata hivyo kutokana na mienendo hiyo uchunguzi uchunguzi wa Mbeya yetu umebaini kuwa usimamizi mbovu wa michango ya fedha za wananchi unatokana na   vijiji vinavyounda kata hiyo kutokuwa na Watendaji hali inayosababisha watu binafsi kukamishwa nyadhifa hizo na kuchangisha michango kisha kutokomea nayo.
  
Kata hiyo inayoundwa na vijiji vtatu ambavyo ni Kijiji cha Magamba, Songambele na Nahalyongo vyote  vikiwa vinasimamiwana makaimu Maofisa watendaji kutokana na kutokuwa na Maofisa wa moja kwa moja waliojariwa na Serikali kushika nafasi hizo.

Aidha kutokana na kukosekana kwa maendeleo katika baadhi ya vijiji  umetokana na usimamizi mbovu wa fedha zinazochangwa na wananchi wenye hali ngumu ya maisha licha ya wakazi hao kupenda kufanya shughuli za maendeleo.

Pia baadhi ya wahusika na wasimamizi wa miradi ndani ya vijiji wameshindwa kufafanua na kuelezea namna ya kukomesha hali hiyo inayorudisha nyuma juhudi za wananchi.

Picha na E. kamanga

Share this article :

0 comments:

 
Support : Creating Website | Greyson Salufu Template | Chimbuko Letu Inc
Copyright © 2011. Kamanga na Matukio - All Rights Reserved
Template Modify by Chimbuko Letu Inc
Proudly powered by Blogger